Utalii wa picha, uwindaji waingiza mabilioni - KATUMA BLOG tz.

HABARI ZA HIVI PUNDE

KWA HABARI ZA UHAKIKA NA KUAMINIKA


Post Top Ad

Responsive Ads Here

Wednesday, August 9, 2017

Utalii wa picha, uwindaji waingiza mabilioni



Image result for Profesa jumanne Maghembe 
WAZIRI wa Maliasili na Utalii, Profesa Jumanne Maghembe amesema utalii wa picha na uwindaji unaofanyika katika hifadhi za taifa na mapori ya akiba nchini yanaliingizia taifa zaidi ya Sh bilioni 50 kila mwaka, huku akibainisha kuwa utalii utaongezeka maradufu mwaka huu.

Aidha, utalii uliingiza asilimia 18 ya pato lote la taifa huku asilimia 25 ya fedha za kigeni zilitokana na utalii uliofanyika katika kipindi cha mwaka uliopita.

Profesa Maghembe amebainisha hayo wakati alipohutubia mkutano wa hadhara katika Kijiji cha Kizi kilichopo katika Wilaya ya Nkasi akiwa katika siku yake ya pili katika ziara yake ya kikazi mkoani Rukwa.

Akiwa njiani kwenda katika Kijiji cha Kizi alisimama kwa muda katika Kijiji cha Lyazumbi na kuzungumza na wananchi, vijiji hivyo viwili vinapakana na Pori la Akiba la Lwafi ambalo lina vitalu vya uwindaji wa kitalii.

Mwaka huu kumekucha utalii unatarajiwa kuongezeka maradufu, muhimu wananchi kwa kushirikiana na askari wa wanyamapori endeleni kulilinda pori hili la akiba ni muhimu sana. Acheni kuvamia na kufanya shughuli za kibinadamu ikiwemo uchomaji mkaa, ufugaji na ujenzi wa makazi, kunasababisha uharibifu mkubwa, amesisitiza.

No comments:

Post a Comment

Post Top Ad

Responsive Ads Here