UWT yampongeza Rais Magufuli bomba la mafuta Tanga - KATUMA BLOG tz.

HABARI ZA HIVI PUNDE

KWA HABARI ZA UHAKIKA NA KUAMINIKA


Post Top Ad

Responsive Ads Here

Wednesday, August 9, 2017

UWT yampongeza Rais Magufuli bomba la mafuta Tanga

Image result for Mwenyekiti wa UWT, amina makilagi

JUMUIYA ya Umoja wa Wanawake (UWT) ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) umepongeza mafanikio ya shughuli ya uwekaji wa jiwe la msingi na kuanza kwa shughuli ya ujenzi wa bomba la mafuta ghafi kutoka Hoima nchini Uganda hadi Tanga.

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Katibu Mkuu wa UWT, Amina Makilagi, bomba hilo lenye urefu wa kilometa 1,445 ambalo litakuwa na uwezo wa kusafirisha mapipa 216,000 kwa siku likiwa na thamani ya Sh tilirioni nane, ni fursa kubwa kibiashara hususani kwa wanawake.

Mradi huu unakadiriwa kutoa fursa za ajira zaidi ya 30,000 kwa wananchi pamoja na kutoa fursa mbalimbali za kibiashara haswa kwa wanawake hii ni hatua kubwa sana kwa nchi yetu hasa kwetu wanawake, amesema Makilagi.

Amesema mradi huo ni hatua nyingine ya kimaendeleo yenye kuimarisha uhusiano wa kindugu na kibiashara baina ya nchi za Afrika Mashariki inayofanikishwa na Rais John Magufuli kwa kushirikiana na Rais Yoweri Museveni wa Uganda.

Aidha, UWT imempongeza Magufuli kwa hatua ya kuwapatanisha Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda na Mkurugenzi wa Vipindi wa Clouds Media, Ruge Mutahaba na kusema kuwa hatua hiyo ni muendelezo wa ujenzi wa taifa la amani lenye watu wenye upendo na walioshikamana.

No comments:

Post a Comment

Post Top Ad

Responsive Ads Here