Mbarali kuanza ujenzi wa zahanati za kata - KATUMA BLOG tz.

HABARI ZA HIVI PUNDE

KWA HABARI ZA UHAKIKA NA KUAMINIKA


Post Top Ad

Responsive Ads Here

Wednesday, August 9, 2017

Mbarali kuanza ujenzi wa zahanati za kata

https://1.bp.blogspot.com/-GOwn7eAPo3E/Vug7vg_gugI/AAAAAAAATtU/qG7EfyCEMfA8Jy8Ghz_mZ_kD_lybwc19A/s400/IMG_0306.JPG

SERIKALI wilayani Mbarali mkoani Mbeya imeagiza vijiji vyote wilayani hapa kuanza ujenzi wa zahanati kuanzia mwezi huu ili kuendana na agizo la serikali la kila kijiji kuwa na zahanati na kituo cha afya kwa kata.



Mkuu wa Wilaya ya Mbarali, Reuben Mfune ametoa agizo hilo kwenye kikao cha Baraza la Madiwani wa Halmashauri ya wilaya hiyo.



Mfune amesema agizo la kila kijiji kuwa na zahanati ni la muda mrefu na ni jambo la kushangaza kuna baadhi ya vijiji havijaanza kutekeleza agizo hilo mpaka sasa.



Amesema jengo la zahanati ni sawa na nyumba ya mtu mmoja hivyo ni jambo lisilowezekana kwa kijiji kizima kushindwa kujenga nyumba hiyo.



Kuanzia mwezi huu kila kijiji kianze ujenzi kama tutashindwa baadaye huko mbele sawa, lakini tuwe tumeonesha nia ya kujenga. Haiwezekani nyumba ya mtu mmoja kijiji kizima kishindwe kujenga.



Nina imani tuna kianzio kizuri kwani kila kijiji kina benki ya tofauti. Tutumie hizo hizo zilizopo kuanza ujenzi. Lakini pia kwa vijiji ambavyo tayari vina zahanati ni wakati wa kuanza mradi mwingine wowote wakati wenzao wakihangaikia zahanati, amesema.

No comments:

Post a Comment

Post Top Ad

Responsive Ads Here