HII NDIO HATIMA YA CUF NA UKAWA - KATUMA BLOG tz.

HABARI ZA HIVI PUNDE

KWA HABARI ZA UHAKIKA NA KUAMINIKA


Post Top Ad

Responsive Ads Here

Wednesday, July 15, 2015

HII NDIO HATIMA YA CUF NA UKAWA



Na Katuma Masamba

Baada ya CCM kumpitisha John Pombe Magufuli, kugombea Urais, kazi kubwa imebaki kwa vyama vya upinzani ambavyo vinaunda Umoja wa Katiba ya Wananchi (Ukawa) kumpata mwakilishi wao.

Story ni kwamba Naibu Katibu Mkuu wa Cuf, Bara, Magdalena Sakaya, amevunja ukimya na kueleza siri  ya Mwenyekiti wa CUF, Prof. Lipumba na viongozi wa kuu chama hicho kutoshiriki kikao cha kumchagua mgombea wa Ukawa.

Sakaya amewaeleza waandishi wa habari leo katika Ofisi za Chama hicho kuwa Cuf, haina mpango wa  kutaka kujiondoa kutoka (Ukawa) na kwamba  maamuzi ya kumpata mgombea wa urais wa umoja huo yatatolewa baada ya kikao cha Baraza Kuu la Uongozi la Taifa la Cuf, Julai 25 mwaka huu.

Chama hicho pia kimekanusha tetesi za kununuliwa na Chama cha Mapinduzi (CCM), ili kiweze kujitoa kutoka Ukawa, hivyo kuudhoofisha umoja huo na kuipa CCM nguvu katika Uchaguzi Mkuu, Oktoba 25 mwaka huu.

Kabla ya kutolewa kwa taarifa hizo, juzi, wanachama wa Cuf, walitinga makao makuu ya chama hicho, Buguruni jijini humo, wakitaka ufafanuzi juu ya habari zilizochapishwa katika baadhi ya mitandao ya kijamii  kwamba, mgombea wa urais wa Ukawa, ameshapatikana na idadi ya kura kutolewa, kinyume cha  utaratibu wa umoja huo.


No comments:

Post a Comment

Post Top Ad

Responsive Ads Here