Waziri asisitiza weledi kwa madaktari - KATUMA BLOG tz.

HABARI ZA HIVI PUNDE

KWA HABARI ZA UHAKIKA NA KUAMINIKA


Post Top Ad

Responsive Ads Here

Tuesday, August 8, 2017

Waziri asisitiza weledi kwa madaktari



Image result for Waziri wa Afya, Mahmoud Thabit KomboBARAZA la Madaktari nchini limetakiwa kufanya kazi kwa kuzingatia maadili na taaluma ya fani hiyo kwa ajili ya kuleta ufanisi na kutoa huduma kwa wananchi.

Hayo yalisemwa na Waziri wa Afya, Mahmoud Thabit Kombo wakati akizindua baraza hilo mjini hapa.

Kombo alisema taaluma ya udaktari, inaheshimika na ni tegemeo kubwa kwa wananchi wengi kwa sababu madaktari wanabeba dhima na majukumu  makubwa.

Alisema Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar chini ya Rais Dk Ali Mohamed Shein, imekuwa ikifuatilia kwa karibu changamoto mbalimbali zinazoikabili sekta hiyo na kuzipatia ufumbuzi.

‘’Macho ya Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar yapo kwa sekta ya afya ikiwemo madaktari kuona maslahi yao yanaboreshwa pamoja na nafasi ya mafunzo mara kwa mara," alisema.

Alisema Baraza la Madaktari ni tegemeo la kuzipatia ufumbuzi changamoto mbalimbali za madaktari pamoja na taaluma hiyo ikiwemo maadili ya kazi.

Alikitaka chombo hicho, kamwe kisiwavumilie madaktari watakaokiuka maadili ya taaluma hiyo kwa kuiondolea heshima yake.

Mwenyekiti wa Baraza la Madaktari, Dk Jamal Adam alisema wamejipanga kuzipatia changamoto mbalimbali zinazowakabili madaktari pamoja na taaluma hiyo.

Kwa mfano, alisema kwa sasa madaktari wanahitaji mafunzo ya mara kwa mara ili kukabiliana na changamoto zinazokwenda na maendeleo ya sayansi na teknolojia katika kutoa huduma za matibabu

No comments:

Post a Comment

Post Top Ad

Responsive Ads Here