Ujerumani kuipiga jeki hospitali ya Tumbi - KATUMA BLOG tz.

HABARI ZA HIVI PUNDE

KWA HABARI ZA UHAKIKA NA KUAMINIKA


Post Top Ad

Responsive Ads Here

Saturday, August 12, 2017

Ujerumani kuipiga jeki hospitali ya Tumbi

1454098034939.jpg
HOSPITALI Teule ya Rufaa ya mkoa wa Pwani ya Tumbi itanufaika na upatikanaji wa vifaa kupitia mradi wa usalama kwa wagonjwa kwa kushirikiana na Chuo Kikuu cha RKU cha nchini Ujerumani.

Akizungumza na mwandishi wa habari hizi ofisini kwake mjini Kibaha, Ofisa habari wa Shirika la Elimu Kibaha ambalo ndilo wamiliki wa hospitali hiyo, Lucy Semindu alisema kuwa mbali ya kunufaika na vifaa pia itanufaika na wataalamu toka chuo hicho.

Semindu alisema kuwa tayari mradi huo umeanza kwa wataalamu kutoka chuo hicho kuitembelea hospitali hiyo wiki iliyopita na kujionea hali halisi ya utoaji huduma.

“Mkataba wa mradi huo uliingiwa mwaka jana utasaidia upatikanaji wa vifaa tiba na kwenye utoaji huduma kuanzia kuwapokea wagonjwa, kuwapatia dawa, upatikanaji wa vifaa vya taka pamoja na kubadilishana uzoefu ambapo wataalamu wa Tanzania nao watatembelea Hospitali ya chuo hicho,” alisema.

Aidha alisema kuwa hospitali hiyo ya Chuo Kikuu RKU ni maarufu kwa kutibu wagonjwa wenye kiharusi na magonjwa mengine, ni tegemeo kubwa kwa Ujerumani na asilimia 100 ya wagonjwa wanaotibiwa ni wa bima na wanapatiwa chakula bure.

No comments:

Post a Comment

Post Top Ad

Responsive Ads Here