Swahili International Tourism Expo kufanyika Dar - KATUMA BLOG tz.

HABARI ZA HIVI PUNDE

KWA HABARI ZA UHAKIKA NA KUAMINIKA


Post Top Ad

Responsive Ads Here

Wednesday, August 23, 2017

Swahili International Tourism Expo kufanyika Dar

Image result for Swahili International Tourism Expo

Na Mwandishi Wetu

MASHIRIKA ya ndege ya nje na ndani yamekubali kushiriki katika maonesho ya ndani ya utalii ili kutangaza utalii wa Tanzania.

Maonesho hayo yanayojulikana kwa jina la Swahili International Tourism Expo yatafanyika jijini Dar es Salaam kuanzia Oktoba 13 hadi Oktoba 15, mwaka huu.

Akizungumza katika hafla ya kutia saini ushirikiano wa kufanikisha maonesho hayo kati ya Bodi ya Utalii Tanzania (TTB) na Shirika la Ndege la Ethiopia, Ethiopian Airlines, Mkurugenzi Mtendaji wa TTB, Devota Mdachi amesema maonesho hayo yanalenga kuitangaza Tanzania kimataifa.

Mbali ya Ethiopian Airlines mashirika mengine ya ndege tunayoshirikiana nayo ni Air Tanzania na Coastal Aviation ambao tufanya nao kazi kwa karibu kuona namna wageni watakavyofikia maeneo ya karibu na vivutio au maeneo husika, amesema Mdachi.

Maonesho hayo yatakayofanyika katika Kituo cha Kimataifa cha Mikutano cha Julius Nyerere (JNICC), mbali ya mambo mengine yatasaidia kutoa taarifa za vivutio vya kiutalii nchini pamoja na mawakala kutoka mataifa mbalimbali kueleza shughuli zao.

Kutakuwa na shughuli mbalimbali ikiwemo ngoma za asili, michezo ya watoto na bidhaa za kitamaduni. Vilevile zaidi ya washiriki 150 watakuwepo kutoka mataifa zaidi ya 15 ikiwemo Kenya, Uganda, Rwanda, Mauritius na Shelisheli, amesema Mdachi.

Kwa upande wake, Meneja Mkazi wa Ethiopian Airlines, Dahlak Teferi amesema wana furaha kuwa sehemu ya wadhamini wa maonesho hayo kwa sababu shirika lao linatazamia kuwa mdau mkubwa wa kutangaza utalii katika ukanda huu wa Afrika Mashariki na Pembe ya Afrika.

No comments:

Post a Comment

Post Top Ad

Responsive Ads Here