Kuku wamtoa roho - KATUMA BLOG tz.

HABARI ZA HIVI PUNDE

KWA HABARI ZA UHAKIKA NA KUAMINIKA


Post Top Ad

Responsive Ads Here

Wednesday, August 23, 2017

Kuku wamtoa roho




Na Mwandishi Wetu, Mwanza



MTU mmoja ameuawa na kundi la watu waliojichukulia sheria mkononi kwa kosa la wizi wa kuku watano wilayani kwimba.



Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mwanza, Ahmed Msangi amesema Agosti 21, mwaka huu saa tatu kasoro robo asubuhi katika kitongoji cha Busulwa, Kata ya Ngulla Wilaya ya Kwimba, Leonard Mathias (23), mkazi wa Kijiji cha Ngulla, aliuawa na kundi la watu waliojichukulia sheria mkononi.



Kamanda Msangi amesema watu hao walimpiga kwa fimbo na mawe sehemu mbalimbali za mwili wake kisha kumchoma moto hadi kupoteza maisha kwa kosa la wizi wa kuku watano mali ya Ester Robert ambaye ni mkazi wa kijiji hicho cha Ngulla.



Inasemekana kuwa mtu huyo aliiba kuku watano nyumbani kwa Ester Robert kisha akakimbilia kijiji cha jirani cha Mwabomba. Inadaiwa kuwa wananchi wa kijiji cha Mwabomba walipomuona akiwa na kuku hao walipata mashaka kisha walimkamata na baadaye walitoa taarifa Kijiji cha Ngulla ndipo mwenye kuku alifika na kukabidhiwa kuku wake.



Inadaiwa kuwa baada ya marehemu kukabidhi kuku kwa mwenye mali, wananchi walimchukua na kwenda naye kituo cha polisi, lakini wakiwa njiani walianza kumshambulia kwa kumpiga fimbo na mawe sehemu mbalimbali za mwili wake na baadaye kumchoma moto. Polisi walipata taarifa kutoka kwa raia wema ndipo walifanya ufuatiliaji wa haraka hadi eneo na tukio na kufanikiwa kukamata watu saba ambao wanadaiwa kuhusika kwa namna moja au nyingine katika mauaji hayo, ameeleza kamanda huyo.



Aidha, Kamanda Msangi amesema kwa sasa polisi wapo katika upelelezi na wanawahoji watuhumiwa saba waliokamatwa kwa kutuhumiwa kuhusika kwenye tukio hilo.


No comments:

Post a Comment

Post Top Ad

Responsive Ads Here