Shambulio la bomu laua watu 24 Kabul, Afghanistan - KATUMA BLOG tz.

HABARI ZA HIVI PUNDE

KWA HABARI ZA UHAKIKA NA KUAMINIKA


Post Top Ad

Responsive Ads Here

Tuesday, August 8, 2017

Shambulio la bomu laua watu 24 Kabul, Afghanistan

Watu 24 wameripotiwa kupoteza maisha nchini Afghanistan baada ya kutokea shambulio la bomu kwenye mji mkuu wa nchi hiyo wa Kabul.

Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi wa Afghanistan, Najib Danish amesema licha ya watu 24 kupoteza maisha kwenye shambulio hilo na wengine 42 wakijeruhiwa.

Polisi nchini humo wamesema tukio hilo lilitokea saa 12:48 asubuhi wakati watu wakielekea kazini na mlipuko ulikuwa mkubwa sana.

Kundi cha Taliban kupitia msemaji wa kundi hilo, Zabihullah Mujahid limedai kuhusika na shambulio hilo ambalo Polisi wamesema ni bomu la kujitoa muhanga na walikuwa wamepanga kulipua mabasi ya ofisi ya Mkurugenzi wa Usalama wa nchi hiyo.

 Baadhi ya majeruhi wa shambulio hilo wakiwa hospitali.

No comments:

Post a Comment

Post Top Ad

Responsive Ads Here