Samia ataka Afrika kuendeleza wanawake - KATUMA BLOG tz.

HABARI ZA HIVI PUNDE

KWA HABARI ZA UHAKIKA NA KUAMINIKA


Post Top Ad

Responsive Ads Here

Saturday, August 12, 2017

Samia ataka Afrika kuendeleza wanawake



MAKAMU wa Rais Samia Suluhu Hassan amesema jukumu kubwa la nchi za Afrika ni kuhakikisha zinaweka mazingira wezeshi ya kuwaendeleza wanawake katika nyanja zote.

Samia ameyasema hayo jana kwenye uzinduzi wa Jukwaa la Kuwawezesha na Kuwaendeleza Wanawake Afrika lililoandaliwa na Asasi ya Graca Machel na kufanyika jijini Dar es Salaam.

Makamu wa Rais alisema pamoja na kuwepo kwa jitihada mbalimbali za kuwaendeleza wanawake bado mazingira hayampi nafasi mwanamke hasa yule anayeishi kijijini.

Aidha, aliainisha baadhi ya changamoto hizo kuwa ni pamoja na sheria na sera zilizopo ambazo bado zinawanyima wanawake fursa ya kumiliki ardhi pamoja na haki ya kurithi hata kama haki hizo zipo kisheria.

Hii inatokana na utekelezaji mbaya wa sheria, unaosababishwa na uwepo wa  mianya ya ubaguzi kwenye kwenye sheria hizo jambo ambalo linakinzana na mfumo rasmi wa kisheria zilizowekwa, alisema.

No comments:

Post a Comment

Post Top Ad

Responsive Ads Here