MKUU WA MKOA ATENGUA MAAMUZI YA BARAZA LA MAAMUZI - KATUMA BLOG tz.

HABARI ZA HIVI PUNDE

KWA HABARI ZA UHAKIKA NA KUAMINIKA


Post Top Ad

Responsive Ads Here

Tuesday, November 29, 2016

MKUU WA MKOA ATENGUA MAAMUZI YA BARAZA LA MAAMUZI

 
Na Eddy Blog, Singida
UJENZI wa Makao Makuu ya Halmashauri ya Wilaya ya Singida, uko njia panda baada ya Mkuu wa Mkoa wa Singida, Mathew Mtigumwe kutengua uamuzi wa Baraza la Madiwani kuhusu ujenzi huo.
Katika kikao cha mwisho cha Oktoba 28 mwaka huu, madiwani walikubaliana kuwa makao makuu mapya ya halmashauri hiyo yajengwe katika kijiji cha Kinyamwambo, kata ya Merya, tarafa ya Ilongero kutokana na eneo hilo kuwa katikati ya halmashauri hiyo kijiografia.
Hata hivyo, Novemba 24 mwaka huu, mkuu wa mkoa huo, alienda katika mji mdogo wa Ilongero na kuitisha mkutano maalumu wa hadhara ambapo alibatilisha uamuzi wa Baraza la Madiwani na kuwahakikishia wananchi wa eneo hilo kuwa, makao makuu mapya yatajengwa hapo Ilongero na si mahali pengine.
Kutokana na matamshi ya Mkuu wa Mkoa, Mwenyekiti wa halmashauri hiyo, Elia Digha, alisema kuwa kauli hiyo ya kutengua uamuzi wa kikao halali cha madiwani ni dharau ya hali ya juu na inalenga kukwamisha ujenzi wa makao mapya ya halmashauri hiyo.
Mwenyekiti huyo ambaye pia ni Diwani wa Msange, alisema kutengua uamuzi halali wa madiwani ni kinyume na Kanuni ya Kudumu ya 3 (3) ya mwaka 2013 ya Halmashauri za Wilaya.
“Inaelekea kuna kitu nyuma ya pazia. Iweje mkuu mkoa aende kwenye mkutano huo muhimu bila kuambatana na mwakilishi yeyote kutoka ofisi ya Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Singida?” Alihoji mwenyekiti huyo.
Akizungumza kwenye mkutano wa hadhara uliofanyika Ilongero hivi karibuni, Mkuu wa Mkoa aliagiza uongozi wa halmashauri ya Singida kuhamia Ilongero ndani ya miezi sita .

No comments:

Post a Comment

Post Top Ad

Responsive Ads Here