WIZARA YA ARDHI YABORESHA UTOAJI HUDUMA - KATUMA BLOG tz.

HABARI ZA HIVI PUNDE

KWA HABARI ZA UHAKIKA NA KUAMINIKA


Post Top Ad

Responsive Ads Here

Tuesday, April 5, 2016

WIZARA YA ARDHI YABORESHA UTOAJI HUDUMA

 Kamishna wa Ardhi Msaidizi Bw. Nathaniel   Methew akiwaeleza waandishi wa Habari leo Jijini Dar es salaam kuhusu kuboreshwa kwa mifumo ya utoaji huduma kwa wananchi kwa kuongeza matumizi ya TEHAMA hali iliyochangia kuongeza  tija  kupitia kituo cha huduma kwa mteja kilichopo  Makao Makuu ya Wizara hiyo na Katika Ofisi  zote za Kanda.kushoto ni Msajili wa Hati Msaidizi
 Msajili wa Hati Msaidizi toka Wizara ya Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Bw. Apollo Laizer akitoa wito kwa wananchi kuzingatia sheria na kanuni wanapotaka kumiliki Ardhi ili kuepusha migogoro ya Ardhi. Kulia ni Kamishna wa Ardhi Msaidizi Bw. Nathaniel   Methew.
Baadhi ya waandishi wa Habari wakifuatilia mkutano wa Wizara ya Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi uliolenga kutoa  ufafanuzi  kuhusu maboresho katika kuwahudumia wananchi kupitia kituo cha huduma kwa mteja.

Frank Mvungi-Maelezo.
WIZARA ya Ardhi , Nyumba na Maendeleo  ya Makazi  imehudumia wananchi 41,932 kati ya Novemba, 2015 hadi sasa   kupitia Kituo cha Huduma kwa Mteja. 

Kauli hiyo imetolewa leo jijini Dar es salaam na Kamishina wa Ardhi Msaidizi  Nathanael Methew wakati wa mkutano na vyombo vya habari, uliofanyika  kwenye ukumbi wa Idara ya Habari(MAELEZO), ambapo alisema lengo la kituo hicho ni  kuongeza tija  na  kasi ya kuwahudumia wananchi.

“Tunahudumia watu zaidi ya 400 kwa siku  na  kwa mwezi ni wateja 8,386 tangu tuanzishe kituo cha Huduma kwa Mteja  hapa Wizarani,” alisema. 
Akifafanua Methew amesema kuwa kituo hicho kimeweza kusaidia kuondoa malalamiko mengi ya wananchi dhidi ya Wizara katika kushughulikia kero na changamoto mbalimbali zinazowakabili wananchi katika sekta ya Ardhi.

Akitaja faida za kituo hicho Methew amesema kuwa kimeongeza imani kwa wananchi na kuondoa uwezekano wa huduma kutolewa kwa upendeleo.
Kituo hicho pia kimepunguza kwa kiasi kikubwa muda ambao wateja wanasubiri kupata huduma.

Katika hatua nyingine Methew amesema kuwa Wizara inao mpango wa kufungua vituo vya huduma kwa wateja kwenye ofisi zote za Ardhi za Kanda.
Naye Msajili wa hati msaidizi Apollo Laizer alitoa wito kwa wananchi kuzingatia sheria na kanuni wanapotaka kumiliki ardhi ili kuepuka migogoro inayohusu sekta hiyo.

Aliongeza kwamba kituo  hicho, kinatoa huduma za utawala wa ardhi,upimaji na Ramani,Mipango Miji na Vijiji,Maendeleo ya Nyumba,Huduma za Usajili wa Hati,  nyaraka mbalimbali na malalamiko ya wateja.

No comments:

Post a Comment

Post Top Ad

Responsive Ads Here