Na Jacquiline
Mrisho-MAELEZO
Waziri wa Nchi Ofisi ya
Rais Manejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Bibi Angela Kairuki
amewapa wiki moja waajiri wa sekta za umma
nchini kukamilisha na kuwasilisha taarifa kuhusu watumishi hewa.
Bibi Kairuki ameyasema
hayo leo Jijini Dar es Salaam alipokua akiongea na waandishi wa habari kuhusu
taarifa za awali juu ya watumishi hewa zilizowasilishwa na Wakuu wa Mikoa
nchini.Hadi sasa taarifa hizo
za Mikoa zimebaini jumla ya watumishi
hewa 1830 ambapo idadi hiyo inazidi kuongezeka kadri utafiti unavyondelea
kufanyika.
“Tunatumia zaidi ya asilimia
51 ya pato la ndani kwa ajili ya mishahara na stahiki za wafanyakazi wa
Serikalini, sasa kama waajiri hawatowataja na kuwasilisha watumishi hewa tutazidi kupoteza pato la
Taifa, Ofisi imewaagiza waajiri wote kuwasilisha taarifa zao wiki hii ili
kuiwezesha ofisi hii na Serikali kiujumla ili kujua kwa usahihi watumishi hewa
ni wangapi na hatua zinazoendelea kuchukuliwa na mamlaka hizo za ajira” alisema
Bibi Kairuki.
Waziri Kairuki
ameongeza kuwabaada ya ukusanyaji wa watumishi hewa kuisha, ofisi yake itafanya
ukaguzi kwenye sekta zote za umma nchini ili kuhakikisha watumishi hewa wote
wanaondolewa pia waajiri watakaokua
hawajawawasilisha watachukuliwa hatua kali za kisheria.
Aidha,Bibi Kairuki
amesisitiza kuwa jukumu la kuwaondoa watumishi sio la ofisi ya Utumishi bali ni
dhamana aliyopewa mwajiri wa sehemu
husika. Hivyo amewataka waajiri kutimiza wajibu wao.
Amewataka waajiri
waambatanishe vielelezo vilivyokosekana katika taarifa za awali za watumishi
hewa vikiwemo; majina, vyeo vyao, vituo vya kazi, namba zao za utambulisho (Check
No) pamoja na sababu za kuwaondoa katika orodha ya malipo.Hatua hii imefanyika baada
ya agizo la Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe
Magufuli alilolitoa Machi 15 mwaka huu alipokua akiwaapisha Wakuu wa Mikoa.
No comments:
Post a Comment