WANAFUNZI WAVUMBUA MIFUKO MBADALA YA PLASTIKI RAFIKI WA MAZINGIRA INAITWA ' ENVIROBAGS - KATUMA BLOG tz.

HABARI ZA HIVI PUNDE

KWA HABARI ZA UHAKIKA NA KUAMINIKA


Post Top Ad

Responsive Ads Here

Wednesday, December 23, 2015

WANAFUNZI WAVUMBUA MIFUKO MBADALA YA PLASTIKI RAFIKI WA MAZINGIRA INAITWA ' ENVIROBAGS

  Vijana Shilen Dawda (kushoto) na Alyanz Nasser wakiwaonesha mifuko hiyo wanahabari wakati wakiitambulisha rasmi Dar es Salaam leo mchana.
 Mkutano na wanahabari ukiendelea.
 Mkurugenzi wa Masoko LTD, Constantine Magavila (kushoto), akitoa ufafanuzi kwa waandishi wa habri katika mkutano huo.
 Mkurugenzi wa Mazingira Ofisi ya Makamu wa Rais, Julius Ningu, akizungumza katika mkutano na waandishi wa habari Dar es Salaam leo mchana katika utambulisho wa mifuko mbadala wa mifuko ya  plastiki inayotunza mazingira ambayo imebuniwa na vijana wawili, Shilen Dawda (kushoto) na Alyanz Nasser (katikati), ambao ni wanafunzi wa Shule ya Kimataifa ya Tanganyika (IST), iliyopo Masaki jijini Dar es Salaam.
 Vijana Shilen Dawda (kushoto) na Alyanz Nasser (katikati), wakimkabidhi , Mkurugenzi wa Mazingira Ofisi ya Makamu wa Rais, Julius Ningu, mifuko mbadala wa mifuko ya plastiki “Rambo), inayotunza mazingira ambayo wameibuni baada ya kuitambulisha rasmi kwa waandishi wa habari Dar es Salaam leo mchana.
Kijana Shilen  Dawda (kushoto), akizungumza katika mkutano na waandishi wa habari Dar es Salaam leo wakati wakitambulisha  mifuko mbadala wa mifuko ya  plastiki inayotunza mazingira ambayo wameibuni na mwenzake  Alyanz Nasser (kulia), ambao ni wanafunzi wa Shule ya Kimataifa ya Tanganyika (IST), iliyopo Masaki jijini Dar es Salaam.

Na Dotto Mwaibale

SERIKALI imewamwagia sifa vijana wawili wakazi wa Dar es Salaam kwa ugunduzi wao unaoenda sambamba na sera ya Serikali ya Awamu ya Tano chini ya Rais John Magufuli ya utunzaji wa mazingira.
Vijana hao ndugu wenye umri wa miaka 14; Alyanz Nasser na Shilen Dawda, wameingiza katika soko la Tanzania aina ya mifuko mbadala ya plastiki ikiwa ni baada ya kufahamu kuwa Tanzania, hususan Dar es Salaam, lipo tatizo kubwa la kimazingira linalohitaji ufumbuzi wa haraka.
Envirobags ni mifuko inayoweza kutumika hata zaidi ya mara tatu tofauti na mifuko ya plastiki iliyopo sasa kwani kinachoshauriwa kwa watumiaji ni kukumbuka kwenda na mifuko hii ya kisasa iwe supermarket au sokoni kufanya manunuzi.
Akizungumza katika hafla fupi ya kuitambulisha mifuko hiyo iliyofanyika jijini Dar es Salaam leo, Mkurugenzi Msaidizi (Idara ya Udhibiti wa Uchafuzi wa Mazingira) wa Ofisi ya Makamu wa Rais, Dk. Julius Ningu, alisema:
“Vijana hawa wameonyesha mfano unaopaswa kuigwa na wadau wote wa mazingira na sisi kama serikali, tunaahidi kushirikiana nao kuhakikisha mazingira yetu yanabaki masafi na salama daima.”
Dk. Ningu aliwataka wadau wengine kujitokeza na kuanzisha miradi ya aina hiyo kwa lengo la kutunza mazingira kwa kuhakikisha Watanzania hawatumii mifuko ya plastiki iliyopigwa marufuku (less 30 microns) na wala haizalishwi.  
Alisema mwaka 2013, serikali ilitunga sheria inayopiga marufuku uzalishaji, usambazaji, uingizaji na zaidi matumizi ya mifuko ya plastiki inayochafua mazingira. Zaidi ya mifuko milioni moja hutumika nchini kila mwaka.
“Ile inayoweza kutumika zaidi ya mara moja ni asilimia ndogo sana na mara nyingi mifuko hiyo hutupwa na kuishia kwenye maeneo kama fukwe za bahari, ambako hudumu kwa zaidi ya miaka 1,000 ikiharibu mfumo wa mazingira,” alisema Dk. Ningu.
Wakizungumza na waandishi wa habari waliokuwapo wakati wa tukio, vijana waliogundua mifuko hiyo, Alyanz na Shilen, walisema walitiwa moyo sana na uamuzi wa rais Magufuli alioufanya mapema mwezi huu wa kuwaongoza wananchi kusafisha jiji.
 “Kutokana na kupigwa marufuku mifuko ya plastiki na juhudi za hivi karibuni za rais kuokoa mazingira, tukaona kwamba ipo haja ya kuwa na mifuko mbadala rafiki wa mazingira. Ni hapo ndipo tukaja na EnviroBags,” alisema Alyanz.
Alisema mifuko hiyo wataiuza kwenye supermarket kubwa nchini wakitarajia kuwa itapunguza matumiza ya kila siku ya mifuko ya plastiki.
“Tunatumaini matumizi ya mifuko hii mipya itakuwa na matokeo chanya kwa taifa letu na hivyo kuweza kuyafikia Malengo ya Maendeleo Endelevu (SDGs),” alisema Shilen kwa niaba ya mwenzake.
(Imeandaliwa na mtandao wa www.habari za jamii.com

No comments:

Post a Comment

Post Top Ad

Responsive Ads Here