SERIKALI YAJIPANGA UPYA KUDHIBITI KIPUNDUPINDU - KATUMA BLOG tz.

HABARI ZA HIVI PUNDE

KWA HABARI ZA UHAKIKA NA KUAMINIKA


Post Top Ad

Responsive Ads Here

Monday, December 28, 2015

SERIKALI YAJIPANGA UPYA KUDHIBITI KIPUNDUPINDU


Na Magreth  Kinabo- MAELEZO.
 
Serikali imeanzisha utaratibu wa utoaji wa taarifa  ya ugonjwa wa kipindipindu kwa wiki  kwa nchi nzima  ili kuweza kuhabarisha umma wa Watanzania kwamba ni mkoa upi au wilaya ipi imejitahidi kukabiliana na ugonjwa huo.

 Utaratibu umeanza rasmi leo, tarehe 28. 12. 2015, hivyo kila Jumatatu  ya wiki  kama leo taarifa za ugonjwa huo zitakuwa zinatolewa.
Kauli hiyo imetolewa leo na Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu wakati akizungumza na waandishi wa habari kuhusu hali ya ugonjwa huo nchini kwenye ukumbi wa mikutano wa wizara hiyo jijini Dar es Salaam.

‘’Ninatoa rai kwa wakuu wa mikoa na wilaya kuhakikisha kwamba wanaleta  taarifa sahihi za watu waliathirika na mlipuko wa  ugonjwa wa kipindupindu kwani kuficha taarifa haitasaidia kwa kuwa ugonjwa huu unaendelea kusambaa katika maeneo mbalimbali ya nchi yetu,’’ alisema Waziri huyo.

Aidha Serikali imesema kwamba   wizara  hiyo kwa itashirikiana na wadau mbalimbali, ambao ni Ofisi ya Waziri Mkuu Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa(TAMISEMI), Wizara ya Maji na Umwagiliaji, Wizara ya Elimu ya Sayansi, Teknolojia na Ufundi, DAWASCO, DAWASA na Sekretarieti ya Mkoa wa Draes Salaam, wakiwemo wadau   wa maendeleo ili kuweza  kukabiliana na ugonjwa huo.

Akizungumzia kuhusu ugonjwa huo, Waziri Ummy alisema  tangu umeanza Agosti 15, mwaka 2015 jijini Dares Salaam,ambapo mpaka Desemba 27, mwaka huu umesambaa katika mikoa 21 ya Tanzania Bara.
 
‘’ Watu  walioathiriwa na ugonjwa huo tangu umeibuka ni 12,222 na jumla ya  watu  196 wamefariki  kutokana na  ugonjwa  huo, lakini mikoa ya Mtwara, Njombe na Ruvuma mpaka hakuna ripoti ya watu waliathiriwa na ugonjwa huo,’’ alisisitiza.

Hata hivyo waziri huyo aliongeza kwamba  katika kipindi cha mwezi nzima mikoa ya Kilimanjaro na Iringa hakuna taarifa za ugonjwa huo, hivyo aliipongeza kwa juhudi walizofanya za kuudhibiti.

 Waziri huyo alifafanua kwamba kwa kipindi cha wiki kuanzia Desemba 21 hadi Desemba 27 mwaka huu jumla wagonjwa 493 wameripotiwa kuugua ugonjwa huo na vifo sita katika wilaya 46 zilizopo kwenye mikoa 18.

 Aliongeza kwamba mikoa inayoonesha kuwa na idadi kubwa ya wagonjwa ni Morogoro(98),  Mara (83), Arusha(60)Singida(48) ,Mwanza (45) na Manyara 27 na mikoa ambayo katika kipindi cha wiki hiyo ambayo haijaathirika na ugonjwa huo ni Iringa, Shinyanga, Kilimanajaro, Pwani na Kagera.

 Aliwataka wananchi kutumia kanuni za afya za kunawa mikono kablaya ya kula, kunywa maji safi  na salama, kuepuka kula vyakula vilivyoandaliwa pasipo kuzingatia  mazingira safi na salama , kuchaemsha maji ya kunywa kuwa vyoo bora ili kuweza kukabiliana na ugonjwa huo. 

Akizungumzia kuhusu suala la uzoaji wa taka kufuatia zoezi la kampeni ya usafi wa mazingira lililofanyika hivi karibuni kwa agizo la  Rais  wa Jamhuri ya  Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli, alisema watashirikiana na TAMISEMI ilikuhakikisha taka hizo zinazolewa. Hata hivyo alisema tayari Waziri husika ameshato siku 21 kukabiliana na tatizo hilo

No comments:

Post a Comment

Post Top Ad

Responsive Ads Here