LIPUMBA AMTEMBELEA RAIS MAGUFULI IKULU - KATUMA BLOG tz.

HABARI ZA HIVI PUNDE

KWA HABARI ZA UHAKIKA NA KUAMINIKA


Post Top Ad

Responsive Ads Here

Monday, November 30, 2015

LIPUMBA AMTEMBELEA RAIS MAGUFULI IKULU


13
Rais Dk. John Magufuli akiwa katika mazungumzo na mgeni wake Prof. Ibrahim Lipumba aliyemtembelea Ikulu

ALIYEKUWA Mwenyekiti wa Chama cha Wananchi CUF Profesa Ibrahim Lipumba, amefungua ukurasa mpya kwa kuwa kiongozi wa kwanza wa kisiasa kumtembelea Ikulu Rais Dkt John Pombe Magufuli na kufanya naye mazungumzo ikiwa ni wiki chache tangu kiongozi huyo alipoapishwa kuongoza nchi.

Kwa mujibu wa taarifa zilizoufikia mtandao huu, katika mazungumzo hayo, Prof. Lipumba ametumia nafasi hiyo kwa kumpongeza Rais Magufuli kufuatia ushindi wake wa kishindo alioupta katika uchaguzi mkuu uliopita.

Mbali na hilo Prof. Lipumba pia ameipongeza hotuba ya Rais Magufuli aliyoitoa wakati wa kufungua Bunge la 11 mjini Dodoma 30, 2015 kutokana na kugusa maeneo mbalimbali yanaaakisi moja kwa moja maisha ya watanzania sambamba na kusimamia uwajibikaji wa viongozi wote.

No comments:

Post a Comment

Post Top Ad

Responsive Ads Here