YOUNG SCIENTISTS TANZANIA (YST) YAENDESHA MAONYESHO YA 5 YA SAYANSI KATIKA UKUMBI WA DIAMOND JUBILEE - KATUMA BLOG tz.

HABARI ZA HIVI PUNDE

KWA HABARI ZA UHAKIKA NA KUAMINIKA


Post Top Ad

Responsive Ads Here

Wednesday, August 5, 2015

YOUNG SCIENTISTS TANZANIA (YST) YAENDESHA MAONYESHO YA 5 YA SAYANSI KATIKA UKUMBI WA DIAMOND JUBILEE


Mkurugenzi Mtendaji na Mwanzilishi Mwenza wa taasisi ya Young Scientists Tanzania (YST), Dk. Gosbert Kamugisha, akizungumza na waandishi wa habari (hawapo pichani) leo hii wakati wa ufunguzi wa maonyesho ya siku tatu ya miradi na ubunifu wa kisayansi uliofanywa na wanafunzi kutoka shule 120 nchini. Maonyesho hayo yatafikia kilele Ijumaa Agosti 7, 2015. (Picha zote na Daniel Mbega wa www.brotherdanny.com).
Mwanzilishi Mwenza wa YST, Joseph Clowry, akisisitiza jambo wakati akizungumza na waandishi wa habari (hawapo pichani) leo hii. 
Makamu wa Rais wa kampuni ya kuchakata mafuta na gesi ya BG Tanzania, John Ulanga, akizungumzia udhamini wao katika maonyesho hayo ya YST. Kampuni hiyo imetoa kiasi cha Dola 200,000 kudhamini maonyesho ya mwaka huu. 
Naibu Balozi wa Ireland nchini, Brian Noran, akizungumzia maendeleo ya tafiti za kisayansi kwa taifa lolote duniani. Kushoto ni Mkurugenzi Mtendaji na Mwanzilishi Mwenza wa YST, Dk. Gosbert Kamugisha. 
Wanahabari wakifuatilia kwa makini. 
Mwalimu Geofrey Ndunguru (kulia) na mwanafunzi Yussuph Mwenda kutoka Shule ya Sekonari ya Wavulana Songea nao wanashiriki maonyesho hayo kuzungumzia Uchambuzi wa Mtazamo wa Wanafunzi Wasioona kuhusiana na Sayansi
Mwanafunzi Gladness Mpelemba (kulia) wa kidato cha tatu kutoka Shule ya Sekondari Sumaye mjini Morogoro akielezea kuhusu utafiti wao wa ‘Kutumia Njia za Asili za Kupanga Uzazi Kupunguza Madhara kwa Wanawake’. Kushoto ni mwenzake Glory Crispine. 
Mojawapo ya utafiti uliofanywa na wanafunzi Saada Abeid na Zaina Maliki wa Shule ya Sekondari ya Wasichana Mtwara. 
Majaji wakiwa kazini leo hii ili kuwapata washindi watakaotunukiwa zawadi mbalimbali hapo kesho ambapo Rais mstaafu wa awamu ya tatu, Alhaj Ali Hassan Mwinyi, ndiye anatarajiwa kuwa mgeni rasmi.
 ………………………………………………..
RAIS mtaafu wa awamu ya pili, Ali Hassan Mwinyi leo anatarajia kuwa mgeni rasmi katika ufunguzi wa maonesho ya kazi za kiugunduzi na kisayansi zilizofanywa na wanafunzi wa shule za sekondari nchini.
Katika uzinduzi huyo, zaidi ya wanafunzi 240 na walimu 120 kutoka bara na visiwani kwa siku tatu wataonesha kazi zao za ugunduzi na utafiti wa kisayansi kama vile kemia, fizikia na hesabu, biologia na teknologia pamoja na teknologia ya jamii.
Mkurugenzi Mtendaji wa Shirikisho la wanasayansi Chipukizi Tanzania (YST) Dk. Gosbert Kamugisha alisema kazi hizo zitajumuisha maeneo mapana ya kisayansi pamoja na kutafuta ufumbuzi kwa masuala kama afya, Kilimo na usalama wa chakula.
Dk. Kamugisha alitaja maeneo mengine kama vile mawasiliano na uchukuzi, nishati na mazingira, elimu, mahusiano na matatizo ya kijamii.
“ Kama njia ya kuwapa moyo vijana wetu wabunifu, zawadi zitatolewa kwa wanafunzi wenye kazi nzuri za kisayansi na teknologia,” alisema Dk Kamugisha.
Naye Makamu Rais wa Kampuni ya uchimbaji wa mafuta na gesi (BG), John Ulanga ambao ndiyo wadhamini wa maonesho hayo alisema zaidi ya wanafunzi 60 watazawadiwa fedha.
Alisema wanafuzi sita watakaoshinda alama za juu watazawadiwa udhamini wa kusoma vyuo vikuu kusomea shahada za sayansi na teknologia na kuendelea kufanya kazi za kisayansi katika maisha yao.
Alisema washindi wa jumla wa maenosho hayo mbali na kupewa pesa na udhamini wa masomo ya vyuo vikuu, pia watashinda zawadi ya kwenda nchini Ireland mwakan kuiwakilisha Tanzaniaa katika mashindano ya kimataifa.
“ YST 2015 ni onesho la wanafunzi wenye vipaji katika sayansi, pia ni ushahidi unaoonyesha kuimalika kwa ujuzi wa walimu ambao ni walezi wa wanafunzi hao,” alisema Ulanga.
Aliongeza kuwa maonesho hayo yataanza kesho (leo) na kumaliza kesho kutwa na yatafanyika katika ukumbi wa Diamond Jubelee na watu wote wanakaribishwa.

No comments:

Post a Comment

Post Top Ad

Responsive Ads Here