KIKWETE KUZINDUA BENKI YA KWANZA YA WAKULIMA TANZANIA - KATUMA BLOG tz.

HABARI ZA HIVI PUNDE

KWA HABARI ZA UHAKIKA NA KUAMINIKA


Post Top Ad

Responsive Ads Here

Wednesday, August 5, 2015

KIKWETE KUZINDUA BENKI YA KWANZA YA WAKULIMA TANZANIA

 DSC_0012
Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya Maendeleo ya Kilimo Tanzania, Thomas Samkyi, akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam kuhusu uzinduzi wa benki hiyo utakaofanyika tarehe 7/8/ 2015. (Kushoto) Mwenyekiti wa Bodi ya Benki hiyo , Bi Rosebud Violet Kurwijila.
DSC_0005
????????????????????????????????????
Mwenyekiti wa Bodi ya Benki ya Maendeleo ya Kilimo Tanzania, Bi Rosebud Violet Kurwijila akizungumza na waandishi wa habari kuhusu uzinduzi wa benki hiyo. Kushoto kwake ni Mkurugenzi Mtendaji wa Benki Thomas Samkyi,
…………………………………………………………
Na Mwandishi wetu- Dar es Salaam
Rais Jakaya Kikwete anatarajiwa kuzindua rasmi benki ya kwanza ya Maendeleo ya Kilimo Tanzania, ambayo inalenga kuanzisha mtizamo mpya wa kukiendeleza kilimo kupitia kushirikisha wadau mbali mbali, kuangalia kila mnyororo wa thamani kwa ukamilifu wake, pamoja na kuwa na ubunifu katika kuchangia kifedha kwenye miradi ya muda mrefu, ya kati na muda mfupi kwenye sekta ya kilimo. Benki hiyo inatarajiwa kutoa mchango mkubwa katika ukuzaji wa sekta ya kilimo ambayo imeajiri zaidi ya aslimia 70 ya Watanzania.
Uzinduzi huo unatarajiwa kufanyika kwa ngazi mbili: ngazi ya kwanza itahusisha uzinduzi wa Makao Makuu ya TADB jijini Dar es Salaam mnamo tarehe 7 ya mwezi huu; ambapo ngazi ya pili itahusisha uzinduzi rasmi wa TADB mbele ya wadau wake wakuu ambao ni Wakulima, kwenye Maonesho ya Nane Nane Mkoani Lindi, katika kilele cha Siku Kuu ya Wakulima hapo tarehe 8 Agosti 2015.
Akizungumza na waandishi wa habari kwenye makao makuu ya benki hiyo yaliyoko Barabara ya Kinondoni, Mkurugenzi Mkuu wa benki, Bwana Thomas Samkyi, alisema dhumuni kuu la uanzishaji wa benki hiyo ni kuboresha tija katika uzalishaji kwenye sekta ya kilimo kwa kuunganisha nguvu za wadau mbalimbali ili kuwezesha uendelezaji wa miundombinu ya kilimo kama miradi ya umwagiliaji, usafirishaji, uhifadhi, mindombinu ya masoko, n.k. ambayo inachangia maendeleo ya sekta ya kilimo.
‘Uanzishwaji wa benki hii unalenga kuziba mianya mikubwa ya ukopeshaji kwenye kilimo ambayo inaachwa na benki za biashara, ili kuchochea kukua kwa sekta ya kilimo, kwa kutoa mikopo na huduma nyingizezo za uwezeshaji wa kilimo kwa wakulima, ambao wengi wao hawana uwezo wa kupata huduma za kibenki’ alisema Bw. Samkyi.
Akieleza zaidi kuhusu uanzishwaji wa benki hiyo, Bwana Samkyi alisema Benki ya Wakulima itakuwa msitari wa mbele katika kusukuma shughuli za kilimo pamoja na kuchagiza benki na taasisi nyingine za kifedha kushiriki katika kuwezesha shughuli za kilimo.
‘Benki hii imeundwa ili kutoa mikopo kwa masharti nafuu, pamoja na kutoa huduma nyinginezo zitakazoongeza uwezo wa wakulima kukopa na kuzalisha. Ili kufanikisha haya, benki inabidi iwe na vyanzo endelevu vya fedha za kutosha kwani nchi hii ni kubwa na wadau wa benki ni wengi sana. Lengo kuu ni kubadili kilimo cha Tanzania kutoka kilimo cha kujikimu kwenda kilimo cha kibiashara’ alisema Bw. Samkyi.
Benki hii pia inatarajiwa kuwa ni kiungo muhimu cha utekelezaji wa mageuzi ya awamu ya pili ya sekta ya kifedha, na vile vile kuboresha maendeleo ya kilimo nchini ikizingatia Dira ya Taifa ya Maendeleo ya 2025 pamoja na mipango mbalimbali ya maendeleo ya miaka mitano mitano, Mkakati wa Maendeleo wa Sekta ya Kilimo, na Mkakati wa Kukuza Uchumi na Kupunguza Umasikini (MKUKUTA), pamoja na sera mbali mbali za Serikali zinazohusu sekta ya kilimo.

No comments:

Post a Comment

Post Top Ad

Responsive Ads Here