UJUMBE WA TAASISI YA NELSON MANDELA KUPANDA MLIMA KILIMANJARO - KATUMA BLOG tz.

HABARI ZA HIVI PUNDE

KWA HABARI ZA UHAKIKA NA KUAMINIKA


Post Top Ad

Responsive Ads Here

Thursday, July 16, 2015

UJUMBE WA TAASISI YA NELSON MANDELA KUPANDA MLIMA KILIMANJARO





UJUMBE maalum wa vijana 37 kutoka Taasisi ya Nelson Mandela Foundation ya Afrika ya Kusini, umeanza safari ya kuukwea Mlima Kilimanjaro.

Lengo la kupanda mlima huo ni kuhamasisha wadau mbalimbali nchini mwao na Pembe ya Afrika kujitokeza kuchangia fedha kuzisaidia familia maskini nchini.

Mkurugenzi wa taasisi hiyo, Sello Hatang, aliiambia NIPASHE jana katika mahojiano maalum kwamba njia pekee ya wao kumuenzi Rais kwanza Mwafrika mweusi kuiongoza Afrika ya Kusini; Nelson Mandela, ni kuzinusuru kaya maskini barani Afrika kwa kuziwezesha kunufaika na sehemu ya michango yake ambayo hutolewa kama fungu maalum la misaada ya kibinadamu.

Alisema mpango wao wa kuichagua Tanzania kunufaika na misaada ya taasisi hiyo kwa kupanda Mlima Kilimanjaro, ni kuzihamasisha taasisi nyingine za utoaji wa misaada ya kibinadamu pamoja na wadau mbalimbali duniani kuona umuhimu wa kutumia vizuri rasilimali walizonazo kusaidia jamii inayowazunguka badala ya kutegemea wahisani kutoka nchini za Magaharibi.


Mhifadhi Mkuu wa Hifadhi ya Taifa ya Mlima Kilimanjaro (Kinapa), Erastus Lufungulo, alisema kuwa idadi ya watalii kutoka mataifa mbalimbali wanaotaka kupanda Mlima Kiliamanjaro, imekuwa ikiongezeka kila mwaka.

Awali, Mkurungenzi wa Hifadhi za Taifa (Tanapa), Allen Kijazi, aliishukuru Taasisi  ya Nelso Mandela, kwa kutambua mchango wa Tanzania kwa nchi ya Afrika ya Kusini wakati wa kupigania uhuru wa taifa hilo na kuamua kurejesha fadhila kwa kuutumia mlima Kilimanjaro, kuchangisha fedha za kuzisaidia kaya masikini lakini pia kuvitangaza vivutio vya utalii vyaTanzania duniani kote.

Kwa mujibu wa Kijazi, ujio wa vijana hao wa Afrika ya Kusini utasaidia kuongeza pato la taifa lakini pia utaingazaTanzania kimataifa kupitia sekta ya utalii.



No comments:

Post a Comment

Post Top Ad

Responsive Ads Here