JESHI LA POLISI KUONGEZA NGUVU KUPAMBANA NA UJAMBAZI - KATUMA BLOG tz.

HABARI ZA HIVI PUNDE

KWA HABARI ZA UHAKIKA NA KUAMINIKA


Post Top Ad

Responsive Ads Here

Thursday, July 16, 2015

JESHI LA POLISI KUONGEZA NGUVU KUPAMBANA NA UJAMBAZI




JESHI la Polisi, Kanda Maalumu ya Dar es Salaam, limeongeza vikosi vingine vya jeshi hilo ili kuongeza nguvu katika mapambano dhidi ya matukio ya uhalifu likiwamo la ujambazi katika kituo cha polisi Stakishari.


Katika tukio hilo  lililotokea Julai 12 mwaka huu kituoni hapo, watu saba wakiwamo askari wanne wa na raia watatu, walipoteza maisha na wengine kujeruhiwa wakiwamo watoto.

Askari akiimarisha ulinzi katika kituo cha polisi cha Stakishari kilichovamiwa na majambazi juzi.

Kamanda wa Kanda hiyo, Suleiman Kova, anasema kuwa operesheni kali ya kuwasaka watuhumiwa wa tukio hilo inaendelea.

Kova anasema wanashirikiana na mikoa mingine ya jirani ikiwamo ya Pwani na Tanga ili kufanikisha msako huo.

Anasema, jeshi hilo limeendelea kupokea taarifa nyingi kutoka kwa wananchi ikiwa ni sehemu ya kuonyesha ushirikiano wao dhidi ya tukio hilo.

No comments:

Post a Comment

Post Top Ad

Responsive Ads Here