VIJANA KUPATIWA MBINU ZA KUPAMBANA NA UMASIKINI - KATUMA BLOG tz.

HABARI ZA HIVI PUNDE

KWA HABARI ZA UHAKIKA NA KUAMINIKA


Post Top Ad

Responsive Ads Here

Thursday, July 16, 2015

VIJANA KUPATIWA MBINU ZA KUPAMBANA NA UMASIKINI

Mkurugenzi wa IYF, nchini, Jeon Hee Yong, akiwa pamoja na mmoja wa vijana waanzilishi wa taasisi hiyo hapa nchini, Yusto akieleza namna alivyobadilika kifikra kupitia Taasisi ya IYF.

VIJANA 3,000 nchini wanatarajia kupatiwa mafunzo ya namna ya kubadili mitazamo yao hasi na kuwa chanya hivyo kuwa kichocheo cha maendeleo katika jamii inayowazunguka.

Mafunzo hayo yatafanyika kwa siku nne mfululizo kuanzia Julai 26 hadi 29, mwaka huu katika ukumbi wa mikutano wa Mlimani City jijini Dar es Salaam chini ya uratibu wa Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo kwa ushirikiano na shirika la kimataifa la IYF tawi la Tanzania.

Akizungumza jijini Dar es Salaam jana, Mkurugenzi wa IYF, nchini, Jeon Hee Yong, alitaja baadhi ya masomo ambayo yatafundishwa katika kambi hiyo ya kubadilisha fikra mpya, kuwa ni uwezo wa kujitambua, tamaa na kujitawala, hekima, mabadiliko  na kushirikiana, moyo na furaha.

"Kambi hiyo ya mafunzo ni kwa ajili ya Watanzania wote kuanzia wenye umri wa miaka 16 na kuendelea wakiwamo walimu huku washiriki watakabidhiwa vyeti vitakavyowasaidia katika masuala ya ajira.

Aliongeza kuwa pia washiriki watapata fursa ya kujifunza lugha mbalimbali za kigeni kikiwamo Kiingereza na Kichina na hivyo kuwasaidia katika kupata ajira.

 


No comments:

Post a Comment

Post Top Ad

Responsive Ads Here