BAYERN HAINA MPANGO NA DI MARIA - KATUMA BLOG tz.

HABARI ZA HIVI PUNDE

KWA HABARI ZA UHAKIKA NA KUAMINIKA


Post Top Ad

Responsive Ads Here

Friday, July 3, 2015

BAYERN HAINA MPANGO NA DI MARIA

KOCHA wa klabu ya Bayern Munich,  Pep Guardiola amesisitiza kuwa, klabu hiyo haina mpango wa kumsajili mchezaji Angel Di Maria wa  Manchester United kwenye msimu huu wa usajili.

Pia aliongeza kuwa fedha zinazotumika kwa ajili ya usajili wa wachezaji wakubwa ni nyingi ambazo hazistahimiliki.

Mchezaji huyo ni moja kati ya wachezaji ambao wamesajiliwa kwa kiasi kikubwa cha fedha, ambapo alipochukuliwa na Manchester United akitokea Real Madrid alichukuliwa kwa kitita cha pauni Milioni 59.7.

Lakini hata hivyo anakabiliwa na changamoto ya kushindwa kucheza kulingana na kitita hicho cha fedha alichonunuliwa.


Kutokana na hali hiyo kumekuwa na tetesi kuwa kuna uwezekano wa klabu hiyo ya Manchester United kuachana na mchezaji huyo na watu wamekuwa wakihisi kuwa huenda angechukuliwa na Guadiola.

Guardiola alisema kuwa kwa upande wake hana haja ya kumchukua mchezaji huyo kwa kuwa tayari kwenye kikosi chake kuna wachezaji wakubwa na wenye uwezo zaidi.

Alisema kuwa tayari imemchukua mchezaji Douglas Costa kutoka Brazil na hawana haja tena ya kuongeza mchezaji mwengine kwa sasa.

Alisema kuwa hana haja ya kumchukua mchezaji huyo kwa kuwa kwanza anajua uwezo wake wa uchezaji na kiwango chake pia na kwa sasa anamuona ni kama mchezaji ambae ni msaada mkubwa kwa timu yake aliyopo ya Manchester United.

"Sioni kama klabu yake hiyo ilifanya kosa kumchukua ila ilikuwa ikijua inachokifanya na uwezo wake ni mkubwa tu hivyo wacha aendelee kutumikia huko."

No comments:

Post a Comment

Post Top Ad

Responsive Ads Here