ACT KUFANYA MKUTANO MKUBWA WA HADHARA KESHO MWEMBE YANGA DAR - KATUMA BLOG tz.

HABARI ZA HIVI PUNDE

KWA HABARI ZA UHAKIKA NA KUAMINIKA


Post Top Ad

Responsive Ads Here

Friday, July 3, 2015

ACT KUFANYA MKUTANO MKUBWA WA HADHARA KESHO MWEMBE YANGA DAR

VIONGOZI wa Chama cha ACT Wazalendo wanatarajia kutoa msimamo wa chama hicho katika masuala mbalimbali ya kitaifa katika mkutano wa hadhara utakaofanyika kesho katika viwanja vya Mwembe Yanga.

Akizungumza na waandishi wa habari kuhusu mkutano huo, Katibu wa Mipango na Mikakati (Taifa), Habibu Mchange alisema, mkutano huo ni kwa ajili ya kukikabidhi chama kwa wakazi wa jiji hilo kama walivyofanya katika mikoa mingine.

Alisema mkutano huo pia utatumika kuwatambulisha wanachama na viongozi wa vyama mbalimbali waliojiunga na chama hicho.

"Mkutano huu utatumika kutangaza na kusisitiza dhamira yetu ya kuwataka Watanzania kuishi katika misingi ya haki, undugu, umoja na mshikamano kwa kutumia miiko iliyowekwa katika Azimio la Tabora linalohuisha Azimio la Arusha," alisema Mchange.

Kwa upande wake, Katibu wa Mambo ya Nje wa chama hicho, Venance Msebo alisema, katika mkutano huo viongozi wa kitaifa wa chama hicho wakiongozwa na Zitto Kabwe watasisitiza msimamo wao wa kushiriki Uchaguzi Mkuu kikamilifu.

"Tumejipanga kusimamisha wagombea katika ngazi zote kuanzia udiwani hadi urais, lakini litatolewa ufafanuzi zaidi katika mkutano huu wa kihistoria utakaofanyika Jumamosi," alisema.

Alisema pia watatoa tamko kuhusu maendeleo ya uandikishwaji wa wananchi katika Daftari la Kudumu la Wapiga Kura  unaondelea nchini.

No comments:

Post a Comment

Post Top Ad

Responsive Ads Here