231 WA CHADEMA WARUDISHA FOMU ZA UBUNGE RUKWA - KATUMA BLOG tz.

HABARI ZA HIVI PUNDE

KWA HABARI ZA UHAKIKA NA KUAMINIKA


Post Top Ad

Responsive Ads Here

Sunday, July 5, 2015

231 WA CHADEMA WARUDISHA FOMU ZA UBUNGE RUKWA



MAKADA 231  wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema)  mkoani Rukwa  wamerejesha  fomu za kuwania  nafasi  za ubunge na udiwani  kupitia  chama  hicho  katika  Uchaguzi  Mkuu ujao.
  
Katibu  wa Chadema  Mkoa  wa Rukwa, Ozem Chapita, alibainisha  kuwa  uchukuaji wa fomu ulianza Mei 18  na kumalizika Juni 25, mwaka huu.

Alisema  kukua kwa demokrasia kumeongeza idadi ya makada wa  chama hicho waliojitokeza  kuchukua  fomu na kuzirejesha kwa wakati  katika  majimbo  yote matano  yaliyopo  mkoani humo.

Alibainisha  kwa nafasi  ya  ubunge  katika majimbo  hayo  matano,  makada  29  walijitokeza kuchukua na kurejesha  fomu  wakiwemo  watano  wa viti maalumu.

“Makada  wa chama chetu  wanaowania   nafasi  ya udiwani ni 143  viti  maalumu  wakiwa  54  hii  ni kwa mkoa  mzima,” alisisitiza.

No comments:

Post a Comment

Post Top Ad

Responsive Ads Here