Saturday, June 20, 2015

FALCAO AKIRI KWENDA CHELSEA



RADAMEL Falcao amebainisha kuwa uhamisho wa mkopo kwenda kwa mabingwa wa Ligi Kuu ya England, Chelsea utakamilishwa katika siku chache zijazo.

Mshambuliaji huyo wa Colombia amekuwa akihusishwa na uhamisho wa mkopo wa muda mrefu kwa Chelsea ambayo kocha wake Jose Mourinho ametangaza kuwa atamnyakua kwa mkopo Falcao.

Mshambuliaji huyo wa zamani wa Atletico Madrid aliichezea Manchester United kwa mkopo msimu uliopita akitokea Monaco.

Hata hivyo, baada ya msimu ambao alifunga mabao manne tu katika mechi 29 kwa mashindano yote, United iliamua kutotumia fursa waliyopewa ya kumsajili kwa mkataba wa kudumu.

Hata hivyo, Chelsea inaonekana kujiandaa kumpa nafasi Falcao ambaye aliwaambia waandishi wa habari: “Ninawaza Copa America na kikosi chetu, wafanyakazi wangu wanashughulikia hilo (la uhamisho).”

Alipoulizwa kama ripoti za uhamisho wa mkopo kwenda Chelsea ni sahihi, Falcao akizungumza baada ya ushindi wa bao 1-0 wa Colombia dhidi ya Brazil, aliongeza: “Inawezekana, mtafahamu hivi karibuni.”

No comments:

Post a Comment