Benki ya Tandahimba yauza hisa - KATUMA BLOG tz.

HABARI ZA HIVI PUNDE

KWA HABARI ZA UHAKIKA NA KUAMINIKA


Post Top Ad

Responsive Ads Here

Wednesday, August 9, 2017

Benki ya Tandahimba yauza hisa

BENKI ya Wananchi wa Tandahimba (TACOBA) mkoani Mtwara imeendelea na mikakati yake ya kujiimarisha kwa kuuza hisa zake ikiwa ni lengo la kuongeza mtaji.



Akizungumza na wananchi wakati wa harambee ya ununuzi wa hisa za benki hiyo iliyofanyika Tandahimba, Meneja Mkuu Benki ya Tacoba, Mgwagi Stephen amsema mipango yote ya kuifanya benki hiyo iwe shindani katika huduma za kibenki nchini imekamilika.



Stephen ameitaja baadhi ya mikakati hiyo kuwa ni kuhakikisha benki inauza hisa zake ndani na nje ya Tandahimba kwa lengo la kuifanya iwe benki ya watu wa kusini.



Katika harambee hiyo iliyokusanya ahadi ya Sh milioni 752, amesema zipo changamoto nyingi zilizojitokeza tangu imeanzishwa, lakini uzoefu umewaonesha kwamba hakuna lisilowezekana. Aliwataka wananchi wote kuchangamkia hisa hizo zinazouzwa Sh 1,000 kila moja.



No comments:

Post a Comment

Post Top Ad

Responsive Ads Here