MAGONJWA mengi hayahitaji tiba. Miili ina njia mbalimbali za kukinga maradhi. Njia hizi ni bora zaidi kuliko kutumia dawa.
Ili kusaidia kukinga na kishinda maradhi ni lazima kujimudu katika hali hizi;
- kujiweka katika hali ya usafi.
- Kula chakula bora.
- Kupumzika vya kutosha
- Kufanya kazi na mazoezi
Hata kama
ugonjwa ni wa kutisha na unahitaji dawa, mwili unaopambana na ugonjwa,
dawa huwa zinasaidia tu. Jambo la muhimu ni usafi, kupumzika na kula
chakula bora.
Huduma za kiafya hazitegemei dawa.
Hata kama
unaishi sehemu ambazo hazina dawa za kigeni, kuna mengi unayoweza
kufanya ili ukinge na kutibu magonjwa mengi mradi tu, uelewe namna ya
kufanya.
Magonjwa mengi yanaweza kukingwa na kutibiwa bila ya kutumia dawa.
Kama watu wanaelewa namna ya kutumia maji vizuri, itakuwa njia nzuri ya kinga na kuponyesha magonjwa bila ya kutumia dawa.
Kuponya kwa maji
Wengi
tunaishi bila ya kutumia dawa lakini, hakuna hata mmoja anayeweza kuishi
bila maji. Ukweli ni kwamba, zaidi ya asilimia 57 ya mwili wa
mwanadamu, ni maji.
Kama kila aishiye vijijini angeweza kutumia maji vizuri, basi magonjwa na vifo hasa kwa watoto wadogo yangepungua sana.
Kwa
mfano, matumizi mazuri ya maji ni msingi wa kuzuia na kutibu ugonjwa wa
kuharisha. Kuharisha ni ugonjwa mkubwa na wenye kuleta vifo kwa watoto
wadogo katika sehemu nyingi ulimwengu. Maji machafu husababisha ugonjwa
huu pia.
Njia
mojawapo muhimu ya kuepuka ugonjwa huu wa kuharisha ni kuchemsha maji ya
kunywa na kupikia hasa kwa ajili ya watoto wachanga.
Chupa ya maziwa na vyombo vingine vya mtoto mchanga, vinabidi pia vichemshwe kabla na baada ya kutumiwa.
Mikono lazima ioshwe kwa sabuni baada ya kutoka msalani, kabla ya kula chakula.
Ukosefu wa maji mwilini ni sababu kubwa ya vifo kwa watoto wenye ugonjwa wa kuharisha.
Kama mtoto anapewa maji mengi yenye chumvi na sukari na asali kidogo, hii itakinga na hata kutibu upungufu wa maji mwilini.
Kumpa
mtoto mwenye kuharisha maji mengi, itamfaa zaidi kuliko dawa. Ukweli ni
kuwa umpapo maji ya kutosha hutahitaji kumpa dawa yoyote ya kutibu
kuharisha.
Nyakati ambazo matumizi mazuri ya maji yanasaidia zaidi kuliko dawa.
Kuhara, minyoo, ugonjwa wa tumbo namna ya kukinga, tumia maji, chemsha maji ya kunywa, osha mikono.
- Ugonjwa wa ngozi
- Oga kila siku
- Vidonda vyenye usaha, pepopunda; osha vidonda kwa maji na sabuni
Kutibu:
Kuharisha na upungufu wa maji mwilini, tumia maji, kunywa maji mengi.
-Homa; Osha kiwiliwili na maji baridi
-Homa kali
-Ogesha kiwiliwili kwa maji baridi
-Mkojo mchafu (hasa kwa akinamama)
-Kunywa maji mengi
-Kukohoa, pumu, nimonia, kifaduro - kunywa maji mengi na fukiza mvuke wa maji ya moto.
-Vidonda, baka la ngozi au kichwa na chunusi
-Sugua kwa maji ya sabuni.
-Madonda ya vijidudu yanayochonota - kanda kwa maji ya moto.
-Maumivu ya misuli na viungo
-Kanda kwa maji moto
-Kuwashwa na malengelenge ya ngozi
-Kanda kwa maji baridi.
Kuungua moto kidogo
- Paweke ndani ya maji baridi.
- Magogore au mafindofindo(sore throat au tonsillitis)
- Sukutua maji moto ya chumvi.
- Esidi au takataka iliyoingia jichoni - osha upesi kwa maji baridi.
Mafua - vuta maji ya chumvi
-Kuvimbiwa na kupata choo kigumu
-Kunywa maji mengi, pia kuinika ni bora kuliko dawa za kulainisha choo. Usitumie mara kwa mara).
Kwa
kila mfano uliotolewa awali,(isipokuwa nimonia), inaonesha kwamba kama
maji yatatumiwa vizuri mara nyingi, dawa hazitahitajika.
Somo hili litapanua mawazo mbalimbali ya kuweza kuponyesa bila kutumia dawa. Tumia dawa tu, kama zinahitajika kweli.
Matumizi mazuri na mabaya ya madawa ya kisasa
Baadhi ya madawa yanayouzwa na mkemia au maduka ya vijijini, husaidia sana.
Watu
wengine wana tabia ya kutumia dawa nzuri vibaya na hii humuumiza
mgonjwa ili dawa iweze kufanya kazi yake ni lazima itumiwe vizuri.
Watu wengi wakiwemo madaktari na waganga, hutoa dawa nyingi kuliko inavyotakiwa na kufanya hivyo, huzidisha magonjwa na vifo.
Kuna hatari katika matumizi ya madawa.
Dawa fulani zina hatari zaidi kuliko nyingine. Lakini, watu wengine hutumia dawa zenye hatari kwa magonjwa madogo madogo tu.
Watoto
wengi wamekuwa wakipoteza maisha kwa sababu mama yake alimpa dawa ya
hatari "Chlorophenical" eti kutibu mafua tu. Usitumie dawa yenye hatari
kwa ugonjwa mdogo.
Mwongozo wa kutumia dawa:
- Tumia dawa tu, ikiwa ni lazima.
- Kila dawa uitumiayo, ni lazima ufahamu matumizi yake barabara na namna ya kujihadhari.
- Hakikisha unatumia kipimo kamili.
- Kama dawa haisaidii au inaleta matatizo, usiitumie tena
- Kama huna hakika, muone mganga.
CHANZO: MZIZI MKAVU BLOG
No comments:
Post a Comment