MNYUKANO MPYA UMEYA KINONDONI, UBUNGO - KATUMA BLOG tz.

HABARI ZA HIVI PUNDE

KWA HABARI ZA UHAKIKA NA KUAMINIKA


Post Top Ad

Responsive Ads Here

Tuesday, September 20, 2016

MNYUKANO MPYA UMEYA KINONDONI, UBUNGO


Aliyekuwa Mstahiki Meya wa Kinondoni, Boniface Jacob


Meya wa Kinondoni, Boniface Jacob jana aliwaaga madiwani wa halmashauri hiyo huku akisema Ukawa imejipanga kunyakua viti vya umeya na naibu wake wa manispaa zaKinondoni na Ubungo, huku wakiwa na idadi ya madiwani wengi.


Ahadi hiyo ya Jacob imeibua vita mpya ya kinyang’anyiro baada ya CCM nayo kutamba kwamba itaibuka kidedea katika halmashauri hizo.

Jacob alieleza jana kwamba kwa idadi kubwa wajumbe wa Ukawa ilionao, umoja huo utaibuka kidedea na kusema itashangaza kama CCM inajipa matumaini ya kushinda wakati idadi ya wajumbe wake ni ndogo.

Akizungumza katika mkutano huo Jacob  mbali ya kuwashukuru wafanyakazi na wananchi  wa Manispaa ya Kinondoni kwa ushirikiano waliompa katika kipindi cha miezi saba(7) aliyodumu kama Meya  alitoa mchanganuo wa Madiwani wa Manispaa  za Ubungo na Kinondoni baada ya kugawanywa jinsi zitakavyokuwa kama alivyochanganua hapa..

SOMA HAPA

Ni dhairi shahiri kuwa Manispaa hizi zitendelea kuwa chini ya UKAWA, na siyo kwa mapenzi binafsi niliyo nayo ila wazungu wanasema "Numbers dont lie" kwa kauli hiyo Manispaa ya Temeke inagawanywa kuwa kigamboni na Temeke,ni dhahiri zote mbili zitaendelea kuwa chini ya CCM,kwakuwa namba hazipo kwenye mapenzi binafsi,ila ukweli CCM wamezidi namba dhidi ya UKAWA.Kiuhalisia na ukweli katika mgawanyo wa Halmashauri zote mbili upo hivi kama ifuatavyo:-

A. HALMASHAURI YA MANISPAA YA UBUNGO.
Katika Manispaa ya Ubungo Chama Cha Demokrasia na Maendeleo(CHADEMA) kina viti vya Madiwani 10 na Idadi ya wabunge wa Majimbo(Ubungo na Kibamba) 2, Chama Cha Wananchi(CUF) kina viti vya Madiwani 2, na Chama Cha Mapinduzi(CCM) kina viti vya Madiwani 2 na Madiwani wa Viti Maalum 2.

Ukiachilia mbali CCM,CHADEMA na CUF katika Halmashauri ya Ubungo havina Madiwani wa viti Maalumu. Kwa hesabu hizo hapo juu katika Halmashauri ya Manispàa ya Ubungo ,CHADEMA inajumla ya Madiwani 10 na wabunge 2 hivyo Jumla kuwa 12, na CUF Madiwani 2,
hivyo kufanya UKAWA kuwa na idadi ya Madiwani 14.Na CCM kuwa na Jumla ya Madiwani 4.
 Hivyo ni wazi kwamba UKAWA wataongoza Manispaa ya Ubungo.

  

 B. HALMASHAURI YA MANISPAA YA KINONDONI.

Katika Halmashauri ya Manispaa ya Kinondoni, Chama Cha Demokrasia na Maendeleo(CHADEMA) kina viti vya Madiwani 8(kawe 5 na Kinondoni 3), wabunge wa Jimbo 1(kawe),Madiwani wa viti maalum 7,na Chama Cha Wananchi(CUF) kina viti 3,Madiwani Viti Maalum 2 na Mbunge wa Jimbo 1(kinondoni) na Chama Cha Mapinduzi(CCM) kina viti 9(kawe 5 na Kinondoni 4),Madiwani wa viti maalum 2 wateule wa Rais 3 na wabunge wa vitu maalum 2.
Kwa hiyo CHADEMA ina viti vya Madiwani 17 na CUF ina viti 7 na CCM ina viti 16, hivyo haihitaji miujiza kujua kuwa kwamba Halmashauri ya Kinondoni itaongozwa na UKAWA. Hii itakuwa na maana 
UKAWA 24
CCM 16

No comments:

Post a Comment

Post Top Ad

Responsive Ads Here