HIZI NDIYO SABABU ZA KIAFYA KWANINI ULE TUNDA LA APPLE - KATUMA BLOG tz.

HABARI ZA HIVI PUNDE

KWA HABARI ZA UHAKIKA NA KUAMINIKA


Post Top Ad

Responsive Ads Here

Thursday, February 11, 2016

HIZI NDIYO SABABU ZA KIAFYA KWANINI ULE TUNDA LA APPLE





"Apple" kwa kiswahili nafikiri linaitwa tunda damu, Tunda hili liko la aina tofauti yako ya kijani yako mekundu na haya mekundu ndio yaliyo mazuri zaidi na pia yanasemakana matunda mazuri zaidi ni yale ya Europe au yale ya Kashmir.

Tunda origin yake ni sehemu za Mashariki mwa Europe na pia Magharibi mwa Asia, na tunda hili linajulikana kwa miaka ya zamani mno katika miji ya Old China, Babulon na Egypt. Tunda hili limetajwa hata katika Quraan na Kitabu cha Nabii Issa A.s

Minerals na viwango vilivyomo katika tunda hilo:
Moisture 84.6% - Calcium 10mg
Protein 0.2% - Phosphorous 14mg
Fat 0.5% - Iron 1mg
Minerals 0/3% - Vitamins A 40 IU
Fibre 1.0% - kiwango kidogo cha Vitamin E,H na B complex
Carbohydrates 13.4%

Tunda hili hutimiwa na lina faida kubwa katika mwili wa mwanaadamu. Lina dawa ya maradhi tofauti:

Anaemia: Apple lina wingi wa iron, arsenic na phosphorus, kwa mtu mwenywe ugonjwa huu inafaa kufanya juice ya apple iwe fresh. Ni vizuri kunywa juice hiyo glass moja kabla kula chakula (nusu saa kabla) na pia kabla ya kwenda kulala usiku.

Kuharisha na kutapika: Mwenye kutokezewa na ugonjwa huu ni vizuri sana kutumia tunda hili (iwe bivu). Kila siku ale 2 pia kama yatapikwa au kuchomwa ni mazuri zaidi kwani hulainisha cellulose.

Dysentery: Kwa watoto aghlabu maradhi haya huwakumba watoto, ni vizuri mtoto akitokezewa na ugonjwa huu kumpa kila wakati kipande cha apple kwani huzuia hali ya ugonjwa huo.

Matatizo ya tumbo: Kuna matatizo tofauti ya tumbo, kwahivo tunda hili limekusanya matatizo yote ya tumbo na kuondoa matatizo hayo. Changanya apple, asali kidogo na ufura kidogo na kula kabla chakula hii husaidia kuondoa matatizo ya tumbo kama vile usagaji mdogo wa chakula na mengine.

Kuumwa na kichwa: Tunda hili lina faida katika maradhi yote ya kichwa. Apple lilowiva limenye maganda yake, halafu ule kwa kutia chumvi kidogo kila siku asubugi kabla ya kula kitu chochote, na uendelee kufanya hivi kwa muda wa wiki 2.

Matatizo ya moyo:Apple ya wingi wa potassium na phosphorus lakini sodium inapatikana kidogo sana.Kwa wakai wa zamani watu walikuwa wakila matunda haya na asali, kwa ajili ya maradhi ya moyo na research imefanyika imeonekana kwa wale watu wanotumia vyakula venye potassium kwa wingi huepukana na maradhi ya moyo. Kwahili ni uzuri kula tunda hili pamoja na asali.

High Blood Pressure:Apple linasaidia katika kuongeza kutoa (secreation) mkojo ambayo hii inasaidia kurudisha blood pressure katika hali ya kawaida, pia inasaidia kupungua kwa sodium chloride katika figo.

Kifua kikavu na kidney stones: 250 grams apple ule kwa muda wa week nzima.

Meno:Matunda haya yanasaidia sana meno katika kuyasafisha na kuyaepusha na vijidudu na kuoza, kila baada chakula kula apple moja.
 
KWA HISANI YA; MZIZI MKAVU BLOG

No comments:

Post a Comment

Post Top Ad

Responsive Ads Here