WATANZANIA WASHAURIWA KUJIONGEZEA KIPATO KWA KUFUGA SUNGURA - KATUMA BLOG tz.

HABARI ZA HIVI PUNDE

KWA HABARI ZA UHAKIKA NA KUAMINIKA


Post Top Ad

Responsive Ads Here

Monday, December 7, 2015

WATANZANIA WASHAURIWA KUJIONGEZEA KIPATO KWA KUFUGA SUNGURA

Mkurugenzi Mkuu wa Kampuni ya Dila Africa, Jumba Dickson akizungumza na waandishi wa habari kuhusu mradi wa ufugaji sungura, wakati waandishi hao walipotembelea kwa mmoja wa wafugaji wa sungura hao katika eneo la Kivungwi, Kata ya Vigazwa Mkoa wa Pwani. KATUMA BLOG tz
 
Dickson akizuingumza na waandishi wa habari waliokuwa kwenye ziara ya mafunzo kuhusu mradi huo.

Mkurugenzi Mkuu wa Dila Africa Co. Ltd Jumba Dickson (kushoto) akiwa amebeba mmoja wa Sungura wanaofungwa kupitia mradi huo. Kulia ni Gladness Nyange Mjasiriamali anayejihusisha na ufugaji wa Sungura.

Gladness Nyange na Jumba Dickson wakiwaonesha waandishi wa habari sungura hao wanaofugwa kupitia mradi wa ufugaji Sungura, nyumbani kwa Gladness.

Baadhi ya Waandishi wa habari wakitembelea katika mabanda yanayotumika kuwafugia Sungura hao.

Baadhi ya Waandishi wa habari wakitembelea katika mabanda yanayotumika kuwafugia Sungura hao.

Dickson akifafanua jambo kuhusu mradi huo mbele ya waandishi wa habari.
 


Na Katuma Masamba, KATUMA BLOG tz
WATANZANIA wameshauriwa kujihusisha na ufugaji wa sungura ili waweze kujiongezea kipato kutokana na mnyama huyo kuwa na faida nyingi.
Faida wakulima wanazoweza kupata kutokana na mnyama huyo mbali na kuuza nyama yake lakini pia wanaweza kuuza kinyesi, mkojo pamoja na ngozi yake.
Ushauri huo umetolewa na Mkurugenzi Mkuu wa Kampuni ya The Dila Africa, Jumba Dickson wakati akizungumza na waandishi wa habari waliokuwa katika ziara ya mafunzo kuhusu mradi huo juzi katika eneo la Kivungwi kata ya Vigwaza, Mkoani Pwani.
Dickson alisema, ufugaji wa sungura unaweza ukawasaidia wakulima katika kujiongezea kipato kwa mbali na kuuza nyama yake lakini pia wana uwezo wa kuuza kinyesi, mkojo pamoja na ngozi yake.
“Tunawafundisha wakulima jinsi ya kufuga sungura ili waweze kunufaika, lakini wanaweza kujiuliza ni wapi wanaweza kuwauza wakishafikia hatua ya kuuzwa, sisi tunawapa soko kwa hiyo kikubwa kwa mkulima ni kufuga tu,” Dickson alisema.
Alisema kampuni yake ina mashamba ya sungura hivyo wanapoingia mkataba na wakulima wanaohitaji kufuga wanakubaliana mambo mbalimbali ikiwemo kuwatafutia masoko ambapo wao wenyewe wananunua sungura hao.
Naye Mjasiriamali na mfugaji wa sungura hao, Gladness Nyange alisema, kuna umuhimu wa akinamama kutumia fursa ya ufugaji sungura ili kumudu kuwasomesha watoto wao badala ya kuwategemea waume zao.
Alisema licha ya kuwa sungura hao wanahitaji uangalizi wa hali ya juu katika kuwafuga lakini amekuwa akihakikisha kuwa waishi katika mazingira mazuri ili waweze kumpa faida.
“Huu ufugaji kwa kuwa ni mpya watu, wengi wanaweza kujiuliza inakuwaje au masoko watapata wapi...lakini mimi nilipoanza kufuga niliingia mkataba na hii kampuni na wao walinipa masoko ina maana kwa kila sungura wa kilo nne nauza kwa Sh 40,000,” Nyange alisema.
Nyange alishauri wajasiriamali na hasa wanawake kujiingiza katika ufugaji huo ili waweze kufanya mambo yao mbalimbali bila kuwategemea akinababa ambao wakati mwingine wanakuwa na majukumu memgi
 

No comments:

Post a Comment

Post Top Ad

Responsive Ads Here