MADEREVA WASISITIZA KUWA WATAGOMA KAMA SERIKALI SIO SIKIVU - KATUMA BLOG tz.

HABARI ZA HIVI PUNDE

KWA HABARI ZA UHAKIKA NA KUAMINIKA


Post Top Ad

Responsive Ads Here

Friday, August 7, 2015

MADEREVA WASISITIZA KUWA WATAGOMA KAMA SERIKALI SIO SIKIVU




 


CHAMA cha madereva wa mabasi na malori nchini, kimesema kitaendelea na mkakati wake wa mgomo nchi nzima, iwapo serikali haitatatua suala la kupatiwa mikataba mipya ya kazi.

Chama hicho kimesema kitakutana na wanachama wote nchini, kesho (Jumapili), ili kutoa tamko la kuitisha mgomo.

Mkutano uliofanyika Juni 21, mwaka huu na uliwakutanisha chama hicho, Wizara ya Kazi na Ajira, Mamlaka ya Udhibiti wa Usafiri wa Majini na Nchi Kavu (Sumatra) na kamati iliyoundwa na Waziri Mkuu, na kutoa maamuzi ya wamiliki kuanza kuwapa mikataba madereva.

Katibu wa chama hicho, Rashid Saleh anasema katika mkutano huo kikao kilipitisha makubaliano ya kuanza kutumika kwa mikataba hiyo, ifikapo Julai mosi, mwaka huu.

Katibu wa Umoja wa Wamiliki wa Mabasi nchini (Taboa), Enea Mrutu, jana alisema kuwa mgomo huo ulipaswa kufikishwa katika kamati iliyoundwa na waziri mkuu, kabla ya kuchukua maamuzi ya kutangaza kugoma.

No comments:

Post a Comment

Post Top Ad

Responsive Ads Here