CUF YAAMUA HAYA,KUHUSU NAFASI ILIYOACHWA WAZI NA LIPUMBA - KATUMA BLOG tz.

HABARI ZA HIVI PUNDE

KWA HABARI ZA UHAKIKA NA KUAMINIKA


Post Top Ad

Responsive Ads Here

Monday, August 10, 2015

CUF YAAMUA HAYA,KUHUSU NAFASI ILIYOACHWA WAZI NA LIPUMBA

SIKU Chache kupita baada ya Profesa Ibrahimu Lipumba kutangaza kujiuzulu nafasi ya uwenyekiti ndani ya  Chama cha wananchi CUF, Hatimaye Chama hicho kimeunda kamati ya mda itakayodumu kwa miezi sita ili kusimamia  nafasi za uongozi .Anaandika KAROLI VINSENT endelea nayo
               
Hatua hiyo imetangazwa mda huu  Jijini Dar es Salaam na Katibu Mkuu wa CUF Maalim Seif ambaye ni Makamu wa Kwanza wa Rais wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar wakati wa mkutano na waandishi wa Habari mara baada ya kumalizika Kikao cha Dharura cha Baaraza la kuu la uongozi wa chama hicho kilichoitishwa kujadili hatua hiyo ya kujiuzulu Profesa Lipumba.

           Ambapo Seif amesema katokana na Kanuni za CUF wamefikia kwa pamoja kuunda kamati maalum itakayosimamia chama kwa kipindi cha Miezi sita na baadae kufanya uchaguzi wa nafasi hiyo ya uenyekiti.
          
Amesema Kamati hiyo itakuwa chini ya Katibu wa CUF ambaye ni yeye Maalim Seif na mwenyekiti wake atakuwa Mbunge wa Afrika Mashariki   Twaha Taslima na Kamati hiyo itakuwa na kazi ya kukijenga chama hicho,pamoja na kushirikiana na Vyama vyengine vinavyounda UKAWA  ambapo anadai itakuwa na jukumu lingine la  kuhakikisha wanaitoa CCM madarakani.

No comments:

Post a Comment

Post Top Ad

Responsive Ads Here