MWINYI ASISITIZA UTUMISHI ULIOTUKUKA - KATUMA BLOG tz.

HABARI ZA HIVI PUNDE

KWA HABARI ZA UHAKIKA NA KUAMINIKA


Post Top Ad

Responsive Ads Here

Thursday, July 9, 2015

MWINYI ASISITIZA UTUMISHI ULIOTUKUKA



RAIS mstaafu wa Awamu ya Pili, Ali Hassan Mwinyi amewataka watendaji wa halmashauri nchini kuendeleza mshikamano na ushirikiano katika dhamira moja ya kuwatumikia wananchi ili waweze kupiga hatua katika maendeleo.

Mwinyi aliyasema hayo jana jijini Dar es Salaam katika hafla ya kuvunja Baraza la Madiwani wa Halmashauri ya Manispaa ya Kinondoni na kusisitiza kwamba sehemu yenye mshikamano ndiyo yenye maendeleo.

Akizungumzia masuala ya kisiasa alisema kuwa, “nchi yetu sasa ipo katika shughuli za kisiasa za kutafuta viongozi bora, lakini Yule mwenye maarifa ni mwenye uzoefu wa kufikia maendeleo.”

Mapema Mkurugenzi wa Manispaa ya Kinondoni, Mussa Natty alisema kwa kipindi cha miaka mitano wameshirikiana mengi na madiwani hao na kufanikiwa kupiga hatua mbalimbali ambapo kwa mwaka 2009/2010 walikuwa wakikusanya Sh bilioni 11.6 lakini kwa sasa wanakusanya Sh bilioni 38.

Kwa upande wake Meya wa Manispaa hiyo, Yusuf Mwenda alisema wamefanya mambo mengi kwa ushirikiano katika sekta ya elimu, afya na maji ambapo pia wanatarajia kutengeneza ajira zaidi ya 1000 katika kiwanda cha kuchakata taka.

No comments:

Post a Comment

Post Top Ad

Responsive Ads Here