MH. LEMA ATAKA SIKU ZA UANDIKISHAJI BVR ZIONGEZWE
MBUNGE wa Arusha Mjini, Godbless Lema ameitaka Tume ya
Taifa ya Uchaguzi (NEC) kuongeza siku za kujiandikisha kwa Mkoa wa Arusha ili
watu wengi waweze kupata nafasi.
Pia
amewataka wasimamizi wa uandikishaji kwa njia ya Biometric Voter Registration
(BVR) nao kuwa makini ili uandikishwaji huo ufanyike kwa kufuata taratibu.
Lema
aliyasema hayo jana wakati akizungumza na Mkurugenzi wa Jiji la Arusha, Juma
Idd pamoja na wenyeviti wa Serikali ya Mitaa.
Katika
mazungumzo hayo pia kulikuwepo na madiwani wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo
(Chadema) ambao walikwenda Ofisi ya Mkurugenzi huyo kulalamikia jinsi
uandikishwaji unavyohujumiwa na baadhi ya watendaji wa kata, waandikishaji wa
BVR pamoja na vifaa kuwa duni..........
Lema
alisema uandikishaji huo umegubikwa na urasimu kwa baadhi ya watendaji wa kata
kwani wanaandikisha wananchi kwa kuangalia kama ni wakazi wa eneo hilo au la.
Alisema
katika maeneo ambayo yana umeme walikubaliana na Mkurugenzi Idd pamoja na watu
wa NEC uandikishaji wa BVR
kuendelea hadi saa 2:00 Usiku,
lakini wahusika hawafuati utaratibu huo.
Alisema maeneo mengine yasiyo na umeme wananchi
wanajitolea kukodisha jenereta ila waandikishaji wanafunga vituo saa 12:00
jioni na kuwaingiza wengine waliobaki katika daftari la Tume ili asubuhi yake
waanze wao wengine wafuate.
Kwa
upande wake, Idd alisema kutokana na tatizo la wingi wa watu ambao
hawakutegemea kama watajitokeza kujiandikisha, NEC imeongeza mashine nyingine
10 za BVR kutoka jijini Dar es Salaam kwa ajili ya kuongeza kasi ya
uandikishaji.
No comments:
Post a Comment