Ofisa Mahusiano wa Tecno Mobile nchini, Eric Mkomoye (katikati) na Meneja wa mitandao Kelvin Boniface wakipokea cheti cha ushindi kwa Tecno Mobile waliyoshinda kupitia Kampeni bora ya mwaka katika mitandao ya Kijamii 2016.
Kampuni inayoongoza
kwa mauzo ya simu nchini Tanzania, TECNO MOBILE imefanikiwa kushinda tuzo za Tanzania Leadership Awards zilizofanyika mwishoni mwa wiki Jijini Dar es
Salaam.
Katika mchakato wa tuzo hizo
zilizoandaliwa na Purple Cow Media,
Tecno iliingia katika tatu bora ikiwa inashindana
na kampuni mbili kubwa nchini Tanzania, kampuni ya mawasiliano ya simu TIGO na kampuni
ya vinywaji TBL , zote zikiwa katika kitengo cha kampeni bora MITANDAO YA
Kijamii ya mwaka katika mitandao ya kijamii.
Tecno waliingia katika kinyang’anyiro
kupitia kampeni yao ya simu maarufu ya TECNO
CAMON C9, katika kampeni iliyoshika
hisia za watumiaji wengi wa mitandao ya kijamii kutokana na kuwapa nafasi watumiaji
wa simu kupiga picha kutokana na maelekezo yaliyokuwa yanatolewa na account za mitandao
ya kijamii ya kampuni, washiriki washindi
walipewa zawadi za aina mbalimbali zikiwemo simu za TECNO CAMON C9.
Tecno imekua kampuni ya kwanza ya simu kushinda
katika kategori hiyo ya kampeni bora ya mwaka ya mitandao ya kijamii kutokana na
uwezo wake mkubwa uliojidhihirisha kwa kuwapa nafasi kubwa watumiaji wa mitandao
na wateja wake kufikisha matzo yao na kusaidiwa lakini pia wateja kuongea na watu
mbalimballi maarufu kama Salma Jabir, Hamisa Mobeto pamoja na Idriss Sultani huku
zawadi kemkem zikitolewa kwenda kwa watumiaji wa mitandao waliofwata TECNO
mobile katika mitandao.
Jamii ya Kitanzania itaendelea kufaidika
na mitandao ya kijamii kupitia kampuni kubwa ya
Tecno Mobile wakifanya matukio mbalimbali ikiwemo kampeni mpya iliyopata
umaarufu ya KAMA MBELE washindi wakipata nafasi ya kwenda kushudia mchezo wa mpira
wa miguu katika jiji la Manchester wakiwa na mchekeshaji Idris Sultan, pamoja na
Kampeni UPENDO inayowataka watumiaji kuweka picha au video katika mitandao ya
kijamii wakisema upendo kwao ni nini na video/picha bora itampa nafasi mshiriki
kuchaguliwa kwenda kusheherekea siku ya wapendao katika hotel kubwa Nchini.
No comments:
Post a Comment