VITENDO VYA UBAKAJI NA ULAWITI VYAONGEZEKA DAR - KATUMA BLOG tz.

HABARI ZA HIVI PUNDE

KWA HABARI ZA UHAKIKA NA KUAMINIKA


Post Top Ad

Responsive Ads Here

Friday, December 30, 2016

VITENDO VYA UBAKAJI NA ULAWITI VYAONGEZEKA DAR

1
Kamishna wa Kanda Maalum  ya Polisi mkoa wa Dar es salaam CP Simon Sirro amesema matukio ya Ubakaji na Ulawiti yameongezeka kwa kiwango kikubwa katika mwaka wa 2016 ukilinganisha na mwaka 2015 kutokana na matukio yaliyolipotiwa kiwa kipindi cha mwaka mzima.
Amesema hii inatokana na kuanzishwa kwa Dawati la Jinsia na pia wananchi kupata uelewa na kuripoti matukio hayo kila yanapotokea hii ndiyo sababu kubwa inayofanya kuongezeka kwa matukio hayo katika mkoa wa Dar es salaam.

Kamishna Simon Sirro akizungumza katika Kituo Kikuu cha Polisi Kati jijini Dar es salaam ametoa  taarifa hiyo wakati  akielezea takwimu za matukio mbalimbali yaliyotokea kwa mwaka 2016,
Kamishna wa Kanda Maalum  ya Polisi mkoa wa Dar es salaam CP Simon Sirro amesema  mwaka 2015 vitendo vya ubakaji vilivyoripotiwa vilikuwa 972 wakati mwaka  2016 vitendo vya kubaka vilivyoripotiwa vilikuwa 1030 ambapo ongezeko lilikuwa ni asilimia 58 ukilinganisha na matukio hayo kwa mwaka 2015.


Akitoa takwimu za vitendo vya kulawiti kwa mwaka 2015 amesema vitendo vya ulawiti vilivyoripotiwa ni 3010 ambapo  mwaka 2016 vitendo hivyo viliripotiwa kwa matukio 383 sawa na asilimia 73.

Amewataka wananchi kuacha matendo maovu kwani hayatawafikisha popote zaidi ya kuishia katika mikono ya sheria na kutupwa jela.
2
Kamishna wa Kanda Maalum  ya Polisi mkoa wa Dar es salaam CP Simon Sirro aksisitiza jambo wakati alipozungumza na waandishi wa habari katika kituo kikuu cha polisi Kati jijini Dar es salaam.
4
Diana Masala Kaimu Mkurugenzi Huduma na Elimu kwa Mlipa Kodi kutoka Mamlaka ya Mapato Tanzania TRA akizungumzia msako uliofanywa kati ya Mamlaka hiyo na Polisi pamoja na vyombo vingine vya usalama ambapo ulifanikisha kukamata bidhaa mbalimbali za magendo.
5
Kamishna wa Kanda Maalum  ya Polisi mkoa wa Dar es salaam CP Simon Sirro akiangalia silaha mbalimbali zilizokamatwa katika misako mbalimbali ya pilisi mwaka 2016.
6
Kamishna wa Kanda Maalum  ya Polisi mkoa wa Dar es salaam CP Simon Sirro akieleza jambo kwa wanahabari wakati alipokuwa akionyesha silaha hizo.
7
Kamishna wa Kanda Maalum  ya Polisi mkoa wa Dar es salaam CP Simon Sirro mitungi ya Shisha iliyokamatwa katika misako hiyo.
8
Kamishna wa Kanda Maalum  ya Polisi mkoa wa Dar es salaam CP Simon Sirro akionyesha moja ya silaha ya kivita zilizokamatwa katika misako hiyo.
9
Baadhi ya maofisa mbalimbali wa polisi wakiwa wametandaza silaha hizo zilizoonyeshwa mbele ya waandishi wa habari.
10
Kamishna wa Kanda Maalum  ya Polisi mkoa wa Dar es salaam CP Simon Sirro akionyesha moja ya bidhaa zilizokamatwa kwa pamoja na jeshi la polisi likishirikiana na Mamlaka ya Mapato TRA kulia ni Diana Masala Kaimu Mkurugenzi Huduma na Elimu kwa Mlipa Kodi kutoka Mamlaka ya Mapato Tanzania TRA.
12
Kamishna wa Kanda Maalum  ya Polisi mkoa wa Dar es salaam CP Simon Sirro akionyesha moja akionyesha moja ya mirija maalum inayotumika kutengenezea pombe haramu ya Gongo.
13 14
Kamishna wa Kanda Maalum  ya Polisi mkoa wa Dar es salaam CP Simon Sirro akionyesha viroba vya bangi iliyokamatwa katika misako hiyo.
15

No comments:

Post a Comment

Post Top Ad

Responsive Ads Here