KICHANGA CHANUSURIKA KUFA KWA MOTO BAADA YA NYUMBA YAO KUTEKETEA HUKO PEMBA - KATUMA BLOG tz.

HABARI ZA HIVI PUNDE

KWA HABARI ZA UHAKIKA NA KUAMINIKA


Post Top Ad

Responsive Ads Here

Monday, June 13, 2016

KICHANGA CHANUSURIKA KUFA KWA MOTO BAADA YA NYUMBA YAO KUTEKETEA HUKO PEMBA

pembaWatu watatu wa familia moja, akiwemo mtoto mchanga wa mwaka mmoja na miezi miwili, wamenusurika kupoteza maisha, baada ya nyumba wanayoishi, kuwaka moto katika kijiji cha Nanguji shehia ya Kendwa wilaya ya Mkoani Pemba.

Moto huo uliotokea majira ya saa 7:00 usiku, wakati familia hiyo ikiwa imelala, ndipo ghafla mama wa familia hiyo Bimkubwa Salim Rashid (23), alipoona mwangaza na kisha kumuamsha mume wake.

Alisema hatua ya kumuamsha mume wake, na kisha kupiga kelele, ndio iliosababisha ndugu, jamaa, marafiki na majirani wa kijiji hicho, kuamka na kuanza kuuzima moto kwa kutumia maji.

Alieza kuwa, ingawa hakukuwa na mtu aliejeruhiwa kwenye tukio hilo, lakini vipo baadhi ya vitu vyao vya ndani viliunga ikiwa ni pamoja godoro na kitanda walichokuwa wamelalia.

“Moto haukuwa mdogo, si unajua nyumba za makuti ikishika moto, lakini majirani wamekuja usiku huo huo, na kutusaidia kuzima, na twawashukuru sana’’,alifafanua.


Nae baba wa familia hiyo Issa Shehe Othaman, alieleza kuwa hajui sababu ya moto huo, kwa vile taa ya kibatali ambayo ilikuwa inawaka, haikuripuka wala kupinduka kama ishara ya chanzo.

Issa alieleza kuwa, wapo baadhi ya majirani na watu wengine wa karibu, waliidai kusikia harufu ya mafuta ya petrol, nusu saa kabla ya kutokea tukio hilo.

“Majirani waliokuwa wakitusaidia kuzima moto, walisema walisikia harufu kali ya mafuta, na kisha ndio wakaona mwangaza mkali wa moto, uliounguza nyumba yangu’’,alifafanua.

Mapema Mkuu wa wilaya ya Mkoani Hemed Suleiman Abdalla, alifika kwenye eneo hilo, na kuitaka familia hiyo kuwa na moyo wa subra, na serikali itakikisha kama kuna yeyote aliehusika atasakwa.

Hemed alifafanua kuwa, sasa serikali imeshachoshwa na vitendo vya kihalifu vinavyoendelea kutokea, na iko tayari kufanya kila njia, ili kuhakikisha wahusika wanafikishwa mbele ya vyombo vya sheria.

“Sisi kama serikali tunaalani vikali matendo haya, na kwa kweli lazima tutumie nguvu kubwa, ili kuhakikisha kama kuna yeyote, basi apatikane, ingawa hatoonewa mtu katika hili’’,alifafanua.

Nae shuhuda aliesaidia kuzima moto huo, Salim Mbarouk Salim alisema baada ya kusikia kelele alitoka nje, na kuona moshi na kusikia moto…moto na kufika kusaidia kuzima.

“Mimi usingizini nilisikia kelele zikinadi juu ya moto, kutoka nje..naam moto unawaka, nikachukua maji na ngazi kupanda juu kuzima’’,alifafanua.
Sheha wa shehia Kendwa Sabiha Mohamed Ali, alisema na yeye alifika usiku huo huo, na kushirikiana na wananchi wake, kuzima moto huo, huku akiitaka familia hiyo kuwa na moyo wa subra.

Tukio la kuungua moto nyumba hiyo, mabyo ni miongoni mwa nyumba 78 zilizowahi kutiwa alama ya X na watu wasiofahamika mwezi Febuari mwaka huu, inalifanya kuwa tukio la tatu, baada ya juzi migomba 129 na mikarafuu tisa kukatwa katwa.

No comments:

Post a Comment

Post Top Ad

Responsive Ads Here