Ndugu Wanaudasa,
Ninasikitika kuwataarifu habari za msiba wa Dr. Richard Mgaya wa Idara
ya Sayansi na Uhandisi wa Kompyuta kilichotokea usiku wa kuamkia jana.
Kwa mujibu wa Mkuu wa Idara (Dr. Honest Kimaro) kifo cha Dr Mgaya
kimesababishwa na ajali ya gari.
Siku ya jana kulisambaa picha kwenye mitandao ya kijamii za gari
lilipopata ajali eneo la Mbezi Afrikana baada ya kugongana na lori na
kuwaka moto. Mashuhuda walishuhudia gari likiwaka moto na hivyo dereva
aliungua moto na kuteketea na hakuweza kutambulika. Hivyo watu
wakasambaza ujumbe kwa kutaja plate number za gari lililoungua ili
kutafuta utambulisho wa dereva.
Kwa masikitiko makubwa, imejulikana kwamba dereva wa gari hilo alikua ni
Dr. Richard Mgaya. Idara ya Sayansi na Uhandisi wa Kompyuta na jamii ya
CoICT kwa ujumla imeshtushwa sana na msiba huu.
Dr. Mgaya alijiunga na idara yetu miaka kama minne hivi iliyopita
akitokoea masomoni Marekani na alikua ni mtaalamu kijana wa Artificial
Intelligence ambayo ni moja ya specialities za computer science zenye
wataalamu wachache sana wa kiwango cha PhD hapa nchini mwetu (kama wapo
zaidi ya yeye). Taarifa za kwamba aliyeungua kwenye gari hili alikua ni
Dr. Mgaya zimeifikia familia yake leo mchana.
Pamoja na ujumbe huu, nimeambatanisha baadhi ya picha zilizopigwa eneo la tukio. Ni msiba mgumu sana kuuelezea na kuukubali.
Mungu mwenyewe awe faraja kwa ndugu, jamaa, wafanyakazi wenzake na familia nzima ya UDSM.
Post Top Ad
Responsive Ads Here
Tuesday, April 5, 2016
Home
Unlabelled
TANZIA: DK RICHARD MGAYA WA IDARA YA SAYANSI NA UHANDISHI WA KOMPYUTA AFARIKI
TANZIA: DK RICHARD MGAYA WA IDARA YA SAYANSI NA UHANDISHI WA KOMPYUTA AFARIKI
About Unknown
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Post Top Ad
Responsive Ads Here
No comments:
Post a Comment