SAKATA LA NDEGE YA SERIKALI NA MAGUFULI,WAKALA WA NDEGE ZA SERIKALI WATOLEA MAJIBU - KATUMA BLOG tz.

HABARI ZA HIVI PUNDE

KWA HABARI ZA UHAKIKA NA KUAMINIKA


Post Top Ad

Responsive Ads Here

Monday, July 20, 2015

SAKATA LA NDEGE YA SERIKALI NA MAGUFULI,WAKALA WA NDEGE ZA SERIKALI WATOLEA MAJIBU


Dk Magufuli, juzi alikwenda Mwanza kwa ziara maalumu ya kujitambulisha akitumia ndege ya Serikali aina ya Fokker F28, jambo ambalo limeibua hisia tofauti.
 

Wakala wa Ndege za Serikali (TGFA) imesema kuwa Chama cha Mapinduzi(CCM) kilimlipia Sh. milioni 8.4 mgombea urais wa chama hicho Dk. John Magufuli kwa ajili ya kutumia ndege ya Serikali kwenda mkoani Mwanza kwenye ziara maalum ya kujitambulisha.

Akizungumza na  Katuma Blog  Ofisa Mtendaji Mkuu wa TGFA, Kapteni Keenan Mhaiki anasema chama hicho kilifuata taratibu zote zinazohusiana na kukodi ndege hiyo na kusisitiza mtu au chama chochote kitakachohitaji huduma ya usafiri hupatiwa kulingana na ratiba  za viongozi wa serikali ambao huitumia kwa safari mbalimbali.

“Hakuna mtu  aliyenyimwa ndege ukiona hajapatiwa kunatokana na ratiba yake kuwa ngumu mara nyingine hutoa huduma ya usafiri timu za mipira zinaposafiri,” alisema Kapteni Mhaiki.

Aidha, anasema ndege hiyo hukodishwa bila upendeleo wa aina yoyote huku akisisitiza hakuna mtu au chama kilichowahi kukodi kikanyimwa bali hutolewa kulingana na nafasi iliyonayo.

Alisisitiza kuwa TGFA itaendelea kufanya jitihada za  kutoa elimu ya matumizi ya ndege za serikali kwa jamii ili kuondoa dhana potofu iliyojengeka kuhusumatumiz 

Julai 19, mwaka huu Dk. Magufuli alitumia ndege ya serikali aina ya Fokker F28 kwenda Mwanza kujitambulisha baada  ya kuchaguliwa kugombea urais na Wajumbe wa  MKutano wa Kamati Maalum ya Halmashauri Kuu ya CCM Taifa( NEC) uliofanyika Julai 12, 2015 mjini Dodoma

No comments:

Post a Comment

Post Top Ad

Responsive Ads Here