ZIDANE AMTAMANI POGBA MADRID - KATUMA BLOG tz.

HABARI ZA HIVI PUNDE

KWA HABARI ZA UHAKIKA NA KUAMINIKA


Post Top Ad

Responsive Ads Here

Friday, June 5, 2015

ZIDANE AMTAMANI POGBA MADRID

GWIJI wa Juventus na Real Madrid Zinedine Zidane amesema Paul Pogba anapaswa kuhamia Hispania kama anataka kuondoka kwa mabingwa wa Italia.

Pogba amekuwa na msaada mkubwa kwa Juvemtus msimu huu hali iliyoibua mjadala wa kutakiwa na timu mbalimbali miezi ya karibuni, na Real ikiwa miongoni mwa timu zinazomuwania.

Na Zidane anayeifundisha timu ya Castilla ya Real alisema Pogba atakuwa amefanya uamuzi sahihi kujiunga na mabingwa hao mara 10 wa Ulaya.

"Sijui ataishia wapi, sina taraifa zake,” alisema mchezaji huyo wa kimataifa wa zamani wa Ufaransa alipozungumza na Radio Monte Carlo.

"Pogba anakiwango cha kucheza anavyotaka, na kwa sasa kama anataka kuondoka Juventus namuomba aende Real Madrid na wachezaji wote bora wanacheza hapa,hivyo nadhani itakuwa nzuri kwake kuja,”.

"Lakini kwa sasa hili si jambo muhimu sana, anamaamuzi yake,”.
Pogba anatarajiwa kuonyesha makali yake kwenye fainali za Ligi ya Mabingwa Ulaya leo ambapo timu yake itacheza na wapinzani wa Real ,Barcelona mjini Berlin.

No comments:

Post a Comment

Post Top Ad

Responsive Ads Here