MBIO ZA URAIS: WALICHOKISEMA PROFESA MUHONGO, WASSIRA NA NYALANDU KIKO HAPA - KATUMA BLOG tz.

HABARI ZA HIVI PUNDE

KWA HABARI ZA UHAKIKA NA KUAMINIKA


Post Top Ad

Responsive Ads Here

Tuesday, June 23, 2015

MBIO ZA URAIS: WALICHOKISEMA PROFESA MUHONGO, WASSIRA NA NYALANDU KIKO HAPA




MMOJA wa makada wa CCM waliojitokeza kuchukua fomu za kuwania urais wa chama hicho, Profesa  Sospeter Muhongo amesema pamoja na utiriri wa wagombea kutoka chama hicho tawala, mwisho wa siku nchi inapaswa kuongozwa na mtu mwenye kuielewa vyema Tanzania na ambaye atakuwa tayari kuivusha nchi kiuchumi.



Aliyasema hayo akiwa Musoma, mkoani Mara wakati akiwashukuru wanaCCM waliojitokeza kumdhamini katika harakati zake za kuisaka Ikulu baadaye mwaka huu, huku akisema pamoja na utayari wake, wamwombee apitishwe na CCM.



“Nchi ni tajiri na hakuna sababu ya kuendelea kuwa masikini. Gesi tutauza nje, madini tutauza nje, nyama na maziwa vyote tutauza nje, tukifanya hivyo itatusaidia kuinua kipato chetu…,” alisema.


Aliwataka Watanzania kuendelea kumwombea kwa Mwenyezi Mungu aweze kumnyooshea safari yake ya kumrithi Rais Jakaya Kikwete anayemaliza muda wake wa kukaa madarakani  kwa mujibu wa Katiba.


WASSIRA
MGOMBEA wa nafasi ya urais ndani ya Chama Cha Mapinduzi (CCM), Stephen  Wassira amesema kujitokeza kwa idadi kubwa ya wanaoomba nafasi hiyo kwa tiketi ya chama hicho inatokana na ukubwa wa CCM, ambayo ina hazina kubwa ya viongozi.


Akichangia hotuba ya Bajeti ya Serikali kwa mwaka wa Fedha 2015/2016 bungeni mjini Dodoma jana kwa kujibu baadhi ya hoja zilizojitokeza wakati wa mjadala, Wassira ambaye pia ni Waziri wa Kilimo, Chakula na Ushirika, alisema CCM ni tofauti na vyama vingine ambavyo idadi ya viongozi wao wakishapanda helikopta hakuna mwingine anayebaki chini.

Alisema CCM ni chama kikubwa chenye demokrasia na wala wananchi wasitishwe na idadi kubwa ya wawania urais CCM ambao sasa wanakaribia 40 na kusisitiza kuwa chama hicho kina utaratibu mzuri unaokubalika na wenye kueleweka kwa jamii kuhusu namna ya kupata viongozi.

“Wingi wa wagombea urais ndani ya CCM unatokana na ukubwa wa chama na kukubalika kwake, tofauti na vyama vingine ambavyo viongozi wake wakishapanda helikopta hakuna tena mwingine anayebaki chini,” alisema Wasira.

NYALANDU

WAZIRI wa Maliasili na Utalii, Lazaro Nyalandu amesema ni lazima Watanzania wanufaike na rasilimali za taifa kabla ya wengine kwa kuwa Mungu amezishusha kwa ajili yao.


Amesema rasilimali hizo ndizo zitatumiwa kuwaendeleza vijana kuongoza na kushika uchumi wa taifa, kwani vijana ndio dili na si bomu kama baadhi wanavyodai.

Nyalandu aliyasema hayo juzi wakati akizungumza na mamia ya wanachama wa CCM waliojitokeza kumdhamini katika ofisi za CCM Mkoa wa Kilimanjaro.

Alisema ni lazima jimbo la Moshi Mjini lirudi mikononi mwa CCM kwa kuwa hakuna sababu ya kushikiliwa na wapinzani.

No comments:

Post a Comment

Post Top Ad

Responsive Ads Here